Shangazi

Sehemu ya KWANZA.

Mwandishi: ASLAM KHAN

Mawasiliano:

                   0627 676104

                   0787 378393

                   0768965020

"Aziza tutaenda wote kuifanya hiyo kazi" nilisema huku nikijribu kuinuka

"Abdam.....abdam!"

"Tulia kwanza unaitwa" mzee aliniambia

"Nani anayeniita?" Nilimuuliza

"Muangalie vizuri anayekuita!"

"Mimi mbona naona?"

"Wewe hauoni, bado kipofu, angalia vizuri utamuona!"

"Abdam..abdam!" Yule mtu aliendelea kuita. Nilipojaribu kuangalia vizuri na taratibu sura ya yule aliyekuwa ananiita ilianza kuonekana vizuri, alikuwa shangazi.

"Vipi, umeamkaje?" Shangazi aliniuliza lakini sikumjibu kitu. Niliangalia kila upande na kujiona kuwa nipo kitandani, hapo ndipo nilipogundua kuwa ile ilikuwa ni ndoto. Nilijaribu kuitafakari sana ile ndoto lakini sikupata maana yake kabisa.

" umenikasirikia kwa sababu nimekutoa kwa aziza?" Shangazi aliniuliza huku akitabasamu

"Hamna shangazi, ni ndoto tu"

"Hahahah bakora yako ni hatari, inachapa hadi katika ndoto, una hatari sana wewe"

" aaah kawaida tu, si unajua nimeshakuwa mtu mzima, kwa hiyo siku moja moja kumwaga maji kitandani sio mbaya!"

"Mmh haya, mimi utanikuta nje!" Alisema shangazi na kutoka nje ya chumba changu.

Niliendelea kuitafakari tena ile ndoto lakini bado nilikosa majibu yake, niliamua kuachana nayo.

Ilikuwa ni siku ya jumatatu iliyo tulivu. Kwa wale waliobahatika kuajiliwa, walikuwa wakielekea katika sehemu zao ili kuwajibika na ujenzi wa taifa. Wakati wengi wao wakienda kazini, hali ilikuwa ni tofauti kwa baadhi ya vijana kwani ndio kwanza walikuwa wakiwaza kwenda kukaa katika vijiwe. Wengi wao wakiwa wanapanga jinsi ya kuongeza mbinu na ujuzi wa kuwaibia wananchi.

Nilitandika kitanda changu vizuri na kufanya usafi katika sakafu kisha nikaanza kupanga panga vitu vizuri viwe katika mpangilio mwengine. Nilipomaliza nilichukua mswaki kisha kuingia bafuni kwa niaba ya kuusafisha mwili wangu kutokana na shombo la samaki aina ya mkunga.

"Aaah mjomba, umeshaamka?" Alikuwa ni mjomba baada ya kukutana nae ukumbini mara baada ya kutoka bafuni, nae alikuwa akielekea bafuni kwa ajili ya kuusafisha mwili na kujiandaa kwenda kazini.

 

"Ndio, nimeamka muda mrefu tu!"

"Vipi maendeleo ya homa?"

"Kwa kweli, namshukuru mungu, naweza kusema nimepona kabisa!"

"Sawa, naenda bafuni, nikirudi, tutaongea!"

"Sawa mjomba!"

Mjomba aliingia bafuni kwa ajili ya kuoga.

"Habari za asubuhi?" Shangazi alinisalimia.

"Mh shangazi, si ulikuja chumbani kwangu, haujanisalimia?"

"Mimi nilikuja kumuangalia huyo akiwa hajaamka anakuaje nimemmiss sana eti!"

"Hebu tuachane na hayo, unajua wewe ni msomi sana eti?"

"Enhe, kwa nini unaniuliza hivyo?"

"Nataka kujua kwani asubuhi zipo ngapi?"

"Asubuhi zipi sasa?" Aliuliza shangazi kwa mshangao. Ulikuwa ni mwendo wa swali kwa swali badala ya swali kwa jibu.

"Aah umeniuliza habari za asubuhi ndio maana!"

"Oooh umeanza utani wako, haya habari ya asubuhi?" Alisema shangazi huku akitabasamu

"Nzuri tu, umeamka salama wewe?"

"Mimi sijambo hofu kwako tu?"

"Mimi nipo vizuri!"

"Naona.........!"

"Kumbe shangazi ukitoka kuamka ndo unakuwa mrembo hivyo?" Nilimtania huku nikimpiga shangazi katika makalio yake makubwa yaliyozuiliwa na khanga moja tu.

"Umeshaanza hivyo, ndio maana mjomba wako huwa hapendi atukute tumekaa pamoja kama hivi!" Alisema shangazi ambaye kiumri alikuwa amenipita miaka mitatu.

"Hapa upo na mimi, yeye anahusika kwa namna gani?" Nilisema huku nikimuangalia shangazi ambaye kutokana na umbo lake lililozuiliwa na khanga moja lilimfanya aonekane ni mrembo zaidi. Kwa sababu alikuwa anafanya usafi, udenda ulikuwa unanitoka kutokana na vile alivyokuwa anainama kwa ajili ya kudeki sakafu. Mambo yalikuwa yanaanza kuharibika. Tayari nguo yangu ya ndani ilikuwa inapambana ili isitobolewe na mkuki wa mmasai aliyekuwa na hasira za kupitiliza.

 

Nini kitatokea.......