Halloween Costume ideas 2015
Articles by "KAZI YA SHETANI"


JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         -KUMI
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

“hebu tuondoke hapa, twende tukakae na wenzetu wanaweza wakatufikiria vibaya!”
“kutufikiria vibaya, kwani kuna mtoto mdogo hapa kati yangu na wewe?”
“hakuna, ila haipendezi, kuwaacha peke yao harafu sisi tunajitenga huku, kama yule mzee akirudi asije kupata tabu tena ya kuanza kututafuta, kwanza alisema tusitoke pale!”
“sawa, wewe ndiye umeshinda, twende!” nilimuambia toka pale katika jiwe na taratibu tukaanza kurejea kule ambako mzee alituacha na kutuambia tusitoke.
“Aziza!”
“ndio!”
“hivi jina lako la kweli ni nani?” nilimuuliza

Endelea…

 “Aziza Abeid Swalehe!”
“wewe ni muislamu kumbe?”
“swadakta (umesema kweli) kabisa!”
“vizuri sana, wewe ni mtoto wa ngapi katika familia yenu?”
“mimi ni mtoto pekee katika familia yetu, baba yangu inasemekana alifariki wakati nilipokuwa na umri mdogo sana!”
“pole sana, je alikuwa anaumwa?”
“hapana, ni ajali tu!”
“ajali ya gari au?”
“hapana, baba yangu alikuwa anaenda kuwatetea wananchi nje ya dunia yetu sehemu moja inayoitwa Kopsheng. Akiwa na wenzake, walizidiwa nguvu na kiongozi wa waasi na badala yake ufalme ukachukuliwa na yule kiongozi wa waasi!”
“aaah, kwa hiyo hata huyo mfalme atakuwa ameuawa?”
“sina taarifa sahihijuu ya hilo, mara nasikia ni mzima mara nasikia ameuliwa, sina uhakika kabisa!”
“dah, pole sana!
“ahsante sana, niliapa lazima nikalipize kisasi cha baba yangu hivyo mama alinipatia mafunzo ya kutumia upanga katika mapambano na kuniambia pindi nitakapofikisha umri wa miaka kumi na nane ndio utakuwa ni umri sahihiwa kulipiza kisasi changu!” 
“sasa una umri wa miaka kumi na nane, utalipizaje kisasi sasa?”
“ndio maana nakuwa mpole sana huku ili niweze kurudi duniani mapema mno nipate kumuuliza mama yangu ni kwa jinsi gani nitakavyoweza kulipiza kisasi na kupata miongozo yote kutoka kwake!”
“kwa hiyo una uwezo wa kupambana kwa kutumia mapanga, si ndivyo?”
“ni kweli, sio hivyo tu bali pia nilifundishwa elimu ya gizani ambayo naweza kuitumia kwa kujillinda na adui!”
“Ina maana unatumia na unaujua uchawi wewe?”
“ndio, je unataka nikufundishe?”
“hapana, hapana, hapana, labda unifundishe kupambana kwa kutumia mapanga tu!”
“njoo ujaribu, ni dakika ishirini tu utajiona jinsi utakavyokuwa, hebu tafuta fimbo ndefu mbili zenye urefu wa mkuki!”
Nilianza kutafuta hizo fimbo kwa takribani dakika tano bila ya mafanikio.
“sijazipata!”
“tumia akili ya kuzaliwa nayo wewe!”
“niambie”
“hii itakuwa ni mara ya kwanza na ya mwisho kukumbusha, umenielewa?”
“sawa!”
“tumia hiko kisu sasa!”
“nakitumiaje sasa?, sijui!” nilimuuliza huku nikiwa nimekishika kisu mkononi.
“acha upuuzi, tumia hisia zako!”
“.......inafanya kazi kutokana na fikra za mtu. Ina uwezo wa kugeuka kila aina ya silaha endapo nafsi yako ikikubalika na nafsi ya hiyo fimbo!” niliyakumbuka maneno ya yule mzee.
Nilikishika kile kisu vizuri na kuweka hisia zangu na kukiamuru kigeuke na kuwa fimbo. Kutahamaki, fimbo nyingi zilitokea na kudondoka chini huku mkononi nikiwa nimebakiwa na fimbo moja.
“upuuzi huu, hhahahahaha!” alisikika Aziza akisema huku akinicheka.
Alikuja na kuninyang’anya ile fimbo niliyobakiwa nayo mkononi na kutahamaki fimbo zote zilipotea na kubakia fimbo moja pale chini. Alinipatia ile fimbo aliyoichukua toka mikononi mwangu na kisha yeye akaokota ile fimbo iliyokuwa ipo ardhini.
“kumbe na wewe una uwezo wa kukitumia hiki kisu?” nilimuuliza kwa mshangao.
“ndio!”
“kwani wewe ni nani?”
“utanitambua baadae, ila si unajua kama mimi ni Aziza?”
“hapana sio hivyo, nahisi kama kuna kitu unachokijua zaidi!”
“wewe ndiye uliyesema, sio maneno yangu hayo. Hakuna kitu chochote ninachokijua zaidi ya kuwa nimepotea huku na inanipasa kurudi nyumbani haraka iwezekanavyo ili niweze kulipiza kisasi kwa wakati muafaka!”
“siamini!”
“hebu shika vizuri hiyo fimbo!” alisema Aziza
Niliishika fimbo yangu vizuri tayari kwa mafunzo.
“kwa sababu wewe pia una nguvu za miujiza tayari, basi haitokuwa kazi ngumu sana!” Aziza aliniambia.
“nguvu za miujiza?, ninazo mimi au?” nilimuuliza kwa mshangao.
“ndio, unazo, ila tatizo ni kuwa hautambui hilo na wala haujui jinsi ya kuzitumia, ila nitakuonyesha!” alisisitiza Aziza.
“duh...!”
“shika fimbo yako hivi...!” alisema Aziza akinionyesha jinsi ya kuishika fimbo vizuri.
“utafuata kwa vitendo kile nitakachokuwa ninakifanya, sawa?”
“sawa!”
“tunaanza, weka mwili wako kama nilivyosimama mimi!”
“sawa.....!”
“kushoto.....kulia.....kati.......kushoto.....”. alisema Aziza huku akiipeleka fimbo yake kulia, kisha kushoto, kisha aliruka kidogo na kuwa kama mtu anayepasua kuni katikati kwa kutumia shoka. Nami nilimfuatisha kwa vile alivyokuwa anafanya.
“......mbele.....nyuma....ngao....ulinzi.....” aliendelea kusema huku ukiinyoosha fimbo yake mbele, kisha akarudisha mikono nyuma kisha akaisimamisha fimbo yake kimshazari na mwili wake. Kila hatua aliyokuwa anaifanya, niliifuatisha kutokana na maelekezo yake. Tuliendelea na yale mazoezi kwa takribani robo saa hivi. Nilitegemea ingekuwa ni mazoezi magumu mno kwangu hasa kutokana na tabia yangu ya kutopendelea kufanya mazoezi mara kwa mara. Lakini mambo yalikuwa ni tofauti kabisa. Nilijiona nilikuwa mwepesi kwa kila ambacho nilikuwa nafikiria kukifanya, tena nilifanya kwa usahihi wa asilimia mia. Kwa kweli nilistaajabu sana!
“vipi Aziza!” ilikuwa ni sauti ya Hamza iliyotustua na kutufanya tukatishe kile tulichokuwa tunakifanya.
“safi tu, karibu!”
“ahsante, naona unampatia mafunzo!”
“yeah, natimiza wajibu wangu!”
“ni vizuri, kwa sababu matatizo yanakuja kuanza muda si mrefu!”
“matatizo?!” niliwauliza kwa mshangao.
“hamna bwana, anatania tu!” alisema Aziza
“hapana, nyinyi kuna kitu munachokifahamu, siwaelewi kabisa yaani!” nilisema kwa kuhamaki.
“huyu mtoto mbishi sana!” alisema Aziza
“muache bwana, atakuja kuelewa baadae, wewe endelea kumfundisha!” alisema Hamza.
“sitaki kufundishwa!”
“kwa nini hautaki?” aliuliza Aziza.
“sina haja ya kujua zaidi, kinatosha kile ulichonipatia!” nilisema
“hapana, bado kabisa!”
“mimi sitaki sasa!” 
“kweli?”
“ndio!”
“mimi nataka tumalizie kama dakika kumi tu!”
“sitaki, inatosha!”
“sogea!” alisema Aziza nami bila ya kubisha nilimsogelea kwa kujiamini. Alinishika kichwa kwa mikono yake miwili na kufanya umbali kati yangu na yeye kupungua. Alisogeza kichwa chake karibu yangu na kuipeleka midomo yake karibu na sikio langu.
“sikia, kama haukijui kile ninachokijua mimi, sahau kupata penzi toka kwangu. Sahau kabisa ndoto za kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mimi. Tena iwe ni ndoto ya mchana ambayo mara nyingi haiwi ya kweli wala haitokei.kikubwa tambua kuwa kauli ya mwisho ndio inayochukuliwa kama ndio amri ya maamuzi jeshini!” alininong’oneza.
                                                                            ***************************


Itaendelea

JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         - TISA
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

“inawezekana wewe unaficha wahalifu!”
“kwa nini nifiche wahalifu wakati najua dawa ya wahalifu ni kitu gani!”
“unajua nini kuhusiana na Tesh?”
“hakuna chochote ninachokifahamu!”
“na kipi unachokifahamu juu ya Tosh?”
“Tosh ni mwananchi ambaye ninamtumia katika mambo yangu binafsi!”
“mambo binafsi?!, mambo gani hayo?, ya kuupindua na kuchukua kinguvu utawala wangu? Hahahahahahahah!” alisema mfalme huku akiwa anacheka kwa kejeli.
“mambo yangu hayahusiani kabisa na uhalifu wala uhaini, Tosh ninamtumia wakati nipo sehemu kama hii, yeye huwa yupo nyumbani kwangu ili kurekebisha na kuiweka nyumba katika hali ya usafi!”
“kwa hiyo Tosh kwa sasa yupo nyumbani kwako?” 

Endelea…

“hayupo!”
“yupo wapi?”
“sipajui pale alipo!”
“acha upuuzi, wewe unaficha wahalifu nyumbani kwako!” mfalme alisema kwa kuhamaki huku akinyanyuka kutoka katika kiti chake cha kifalme.
Taratibu maumbile ya mfalme yalianza kubadilika na kuwa kiumbe wa ajabu. Hali hii iliwafanya wajumbe waliokuwepo pale kuanza kuingiwa na woga. Alianza kuwa na umbile kubwa na taratibu kucha za miguu na mikono zilianza kuchomoka na kuwa ndefu. Meno nayo yalikuwa kama ya kiumbe anayekula nyama. Masikio yalikuwa marefu kama fey na mbawa zilianza kumtoka. Waziri Kopsha alivyoona vile, nae akaanza kubadilika ili kuwa tayari kujitetea kwa kile kitakachotokea. Waziri alikuwa nyoka mkubwa sana mwenye pembe mbili kichwani na miguu sita. Wakati mfalme akiwa anamwelekea waziri Kopsha, mmoja wa wasaidizi wake alienda na kumnong’oneza jambo hali iliyomfanya mfalme kubadilika kurudi katika hali yake ya kawaida na akarudi kukaa pale katika kiti cha enzi cha kifalme huku akiwa amejawa na hasira. Waziri Kopsha nae alirudi katika umbile la kawaida na kwenda katika sehemu yake na kukaa.
“wajumbe tunaomba radhi kwa kile kilichotokea hapa ila tunapenda kuwataarifu kuwa mkutano umeisha kwa leo. Pindi mutakapohitajika tena mtataarifiwa” alisema msaidizi wa mfalme na kisha mfalme na wasaidizi wake wakaondoka. Kwa kile kilichotokea, hakuna hata mmoja aliyekumbuka kuhusu watu waliotakiwa kuuliwa kwa makosa yausaliti. Wajumbe na washirka wote walindoka katika eneo la mkutano huku kila mmoja akiwa na jambo la kusimulia katika familia zao.
                                                     ********************************
Tulikaa pale mara baada ya yule mzee kuondoka kuelekea katika mkutano. Tuliangalia angalia katika eneo lile ambalo lilikuwa ni eneo zuri sana. Tulianza kuzunguka zunguka ili kuangalia na kufurahia uzuri wa eneo lile la bustani. Ukubwa wa bustani hii, ulikuwa sawa na ukubwa wa kiwanja cha mpira wa miguu au zaidi yake. Nilipokuwa naendelea kuzunguka katika ile bustani, nilimuona Aziza akiwa katika eneo lenye vipepeo wengi sana. Alikuwa amekaa chini akionekana kufurahia upepo mwanana wa sehemu hii. Niliamua kumfuata ili kuongea nae mambo kadhaa.
“vipi Aziza?”
“poa, niambie!”
“naona unakamata vipepeo hapa?!”
“yeah!, unapenda na wewe kucheza na vipepeo?”
“aaah, mimi sio mtoto kama wewe!”
“hahahahaa kwa hiyo mimi ni mtoto, sio?
“kwani haujioni kama wewe ni mtoto kuliko mimi?”
“una ukubwa gani wewe mwanaume?” alisema Aziza huku akiinuka na kusimama kisha kuniangalia usoni.
“wewe ni mtoto kabisa kwangu!”
“sema tu    unataka ubishi wewe!”
“sio ubishi, una miaka mingapi?”
“kumi na minane!”
“sasa si nilikuambia wewe ni mdogo kabisa kwangu?”
“kwani wewe una miaka mingapi?”
“ishirini na tatu!”
“kwa hiyo miaka ishirini na tatu tu, unajiona mkubwa sana eeeh?”
“kwani hauoni ni miaka mingapi niliyokupita?”
“mitano!”
“sasa je, waonaje?”
“hauna ukubwa huo hata kidogo!”
“unaniweza mimi?”
“kukuweza kivipi?”
“nakuuliza mimi ni saizi yako?”
“hata ungekuwa na miaka ishirini na nane, bado ungekuwa ni saizi yangu tu!”
“kivipi?”
“hivyo hivyo unavyomaanisha wewe!”
“kama……!”
“vyovyote vile unavyofikiria!” alisema Aziza wakati tukiwa tunatembea tembea katika bustani. Tulienda katika sehemu ambayo kilikuwa na maporomoko ya maji. Tulitafuta sehemu moja iliyo nzuri ili tuketi. Tulikaa juu ya jiwe moja huku tukiangalia maji yaliyokuwa takitiririka Taratibu. Ajabu katika maporomoko haya, yalikuwa ni maji yaliyokuwa kama mvua tu kwa sababu hakukuwa na mlima ingawa maji haya yalikkuwa yakidondoka kama katika maporomoko mlimani. Ilikuwa ni eneo linalovutia sana.
“kuwaza kama vipi?” nilimuuliza
“kwani wewe unawaza nini?”
“unanipenda?”
“ndio nakupenda!”
“kweli?”
 “kwanza unamaanisha kivipi?”
“wewe unanipendaje kwani?”
“kibinadamu, kama watu ambao tupo katika matatizo pamoja, tupendane ili tupate msaada pamoja!”
“anha kumbe?”
“ndio hivyo, au wewe una kitu za ziada unataka kuniambia?”
“hapana!”
“kweli?”
“waangalie hao wanaokuja huku!” nilimwambia Aziza huku nikimuonyesha ujio wa Shebby na Tina.
“aaaah wapendanao hao!” alisema Shebby.
“nawaona hapo!” nilisema
“naona hapo mpaka kitaeleweka tu, muda wote huo mliokaa hapa?” alitania Shebby.
“aah wapi, hanipendi huyu!” nilisema huku nikimuangalia Aziza
“mmmh ndivyo nilivyokuambia?” aliuliza Aziza kwa sauti ya chini, sikumjibu.
“munaenda wapi huku?” niliwauliza
“tumesikia bwana, mjibu mwenzako huko!” alisema Tina.
“nitamjibu!” nilisema.
“hahahahahahaha anaona aibu mwanaume mzima, hebu tuondoke Tina tuwaache kama kweli atamjibu!” alisema Shebby huku akimshika mkono Tina na kuondoka katika eneo tulilokuwa tumekaa.
“enhe, niambie!” nilimwambia Aziza mara baada ya Shebby na Tina kuondoka katika eneo lile.
“nikuambie kitu gani?”
“wewe si ulisema haujaniambia?”
“kukuambia kitu gani?”
“pale niliposema haunipendi, wewe ukasema haujaniambia kama haunipendi!”
“sasa je, kwani nilikuambia?
“kwa hiyo unanipenda?”
“ndio!”
“kivipi!”
“nafikiri tayari nilishakuambia kabla!”
“mimi Sitaki kama ulivyoniambia muda ule!”
“wewe unatakaje?”
“kimapenzi!”
“unasemaje?”
“nakupenda uwe mpenzi wangu!”
“Mpenzi wako?, yaani mimi na wewe tuwe katika mahusiano ya kimapenzi?”
“ndio!”
“usinifurahishe bwana, enhe ni kwa kipindi gani?”
“kipindi chote tu!”
“shida yako unifanye mimi mdoli wa kunichezea, sio?”
“hapana, sina nia hiyo kabisa!”
“kama hauna nia hiyo, sasa hivi tukirudi katika dunia yetu utawezaje kuniona mimi, hebu acha kuchekesha watu bwana!”
“dah!”
“dah kitu gani?”
“kwa hiyo haiwezekani?”
“haiwezekani na inawezekana pia!”
“kwa nini isiwezekane na iwezekane kwa pamoja?”
“haiwezekani kwa sababu Sitaki kuwa na mahusiano na wewe, sihitaji kuchezewa kabisa!”
“duh, enhe!”
“inawezekana kwa sababu mimi ni mwanamke!”
“sijakuelewa kabisa, nieleweshe basi!”
“hebu tuondoke hapa, twende tukakae na wenzetu wanaweza wakatufikiria vibaya!”
“kutufikiria vibaya, kwani kuna mtoto mdogo hapa kati yangu na wewe?”
“hakuna, ila haipendezi, kuwaacha peke yao harafu sisi tunajitenga huku, kama yule mzee akirudi asije kupata tabu tena ya kuanza kututafuta, kwanza alisema tusitoke pale!”
“sawa, wewe ndiye umeshinda, twende!” nilimuambia toka pale katika jiwe na taratibu tukaanza kurejea kule ambako mzee alituacha na kutuambia tusitoke.
“Aziza!”
“ndio!”
“hivi jina lako la kweli ni nani?” nilimuuliza
Itaendelea…

JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         - NANE
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

“ Ila naomba mtambue kuwa sio kila unayemuona ana mafanikio, ana mali nyingi au maarufu sana sio kama amepatia huku mafanikio, la hasha! Wengine ni bidii ns juhudi zao ndizo zilizowafanya wafanikiwe!” alimaliza na kutufanya tujenge taswira na kuanza kuwafikiria watu maalufu wengine wakipata umaarufu kwa vitu vya kipuuzi.
“huyo kiongozi wa zamani yupo hai au ameshakufa?” niliuliza
Ýupo hai mpaka leo, uzuri wake ni kuwa ni kuwa hakuna kati ya viumbe wabaya wenye kujua pale alipo, ila kila siku wanaishi naelakini hawamjui. Kila siku wanamtafuta kwa udi na uvumba kwa kujua kuwa kuna sehemu alipojificha!” alijibu.
“wewe unamjua?” Shebby aliuliza. Yule mzee alimuangalia Shebby kwa makini kwa sekunde kadhaa.

Endelea...

“hapana, simtambui” alijibu yule mzee.
“wewe ulijuaje kama yupo hai mpaka leo na anaishi pamoja na watu wanaomtafuta?”
“nitakuja kujibu maswali yenu baadae, naomba niondoke, muda wa mkutano umeshawadia, kwa hiyo ngojeni niende kwanza!” alisema yule mzee na kuondoka. Baada ya dakika moja alirudi tena
“nilisahau, nawaomba msitoke, nitarudi muda si mrefu mkutano ukimalizika tu, mmenielewa?
“ndio!”
Tulipomjibu akaondoka katika eneo lile.
                                      *********************************************************************
Kama ilivyo ada ya kila mwezi katika nchi ya Kopsheng, kunakuwa na mkutano wa kujadili mambo mbalimbali yaliyotokea na yanayoendelea kutokea huku baadhi ya  wajumbe wakipewa nafasi ya kutoa maoni yao kuhusu hali ya ufalme na utawala wake ulivyo na mapendekezo ni kwa namna gani wangependa uendeshwe ili kuleta maendeleo katika nchi yao. Hakuna hata mmoja ambaye hudiriki kusema ukweli kuhusu jinsi ambavyo wananchi wanavyoishi na vile wanavyouzungumzia utawala huo. Wengi wao husema wananchi wanafuraha na wanafurahia jinsi utawala unavyoendelea ili kuepusha kupoteza nafsi zao.miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na wajumbe ambao walikuwa wakiyapeleka moja kwa moja yale wanayoyasema wananchi juu ya utawala mbovu wa mfalme huyo. Kilichofuata kwao ni mauaji ya kikatili ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa kwa mifupa yao kwa kutumia nguvu kubwa ya maajabu na kujenga chumba maalumu kinachounganisha kiwanda cha kutengenezea jeshi la wafu na nchi ya Kopsheng. Kilikuwa ni chumba cha siri ambacho kilifahamika na baadhi tu ya washirika wa karibu wa mfalme. Tofauti na jeshi lililokuwa likifahamika na wananchi wa Kopsheng, bado alikuwa na jeshi kubwa la siri lililokuwa linaishi chini ya ardhi.
Wajumbe wengi walifurika ili kujua nini kitaongelewa na mfalme. Baada ya wajumbe na wawakilishi kuwasili katika eneo la mkutano, msaidizi wa mfalme alifungua mkutano.
“mabibi na mabwana, kama ilivyo ada yetu ya kila mwezi, tumekutana hapa ili kuweza kujadili kuhusu maendeleo na matatizo yanayoikabiri Kopsheng. Lakini mpaka muda huu bado waziri wetu hajawasili kwa hiyo tutasubiri kidogo kabla ya mkutano wetu kuanza, wakati huo mfalme wetu kuna mambo anayamalizia!” alisema mmoja wa watu wa karibu na mfalme. Baada ya dakika kadhaa, mfalme akiwa na wasaidizi wake waliwasili katika eneo la mkutano. Kwa hali ambayo haikuzoelewa, sehemu ya waziri ilikuwa tupu.
“je, kuna taarifa gani kuhusu waziri Kopsha?” aliuliza mfalme
“hatujapokea taarifa zozote kuhusu yeye mpaka sasa hivi!” alijibu mmoja wa viongozi wasaidizi wa mfalme.
“walinzi...........!”
“...ndio mfalme.....!”
“siku nyingi nina mashaka na huyu mzee, nendeni popote mutakapomkuta mukam........!” kabla mfalme hajamaliza kauli yake, waziri Kopsha aliingia katika sehemu ya mkutano hali iliyowafanya wajumbe na wawakilishi wote kusimama isipokuwa washirika wa karibu wa mfalme. Jambo hili lilikuwa likimchukiza sana mfalme. Waziri alipoketi, ndipo wajumbe na wawakilishi wananchi nao wakaketi.
 “mbona umechelewa sana kufika katika mkutano waziri na sio kawaida yako?” mfalme alimuuliza waziri Kopsha ambaye alibakia kimya tu pasi na kujibu kitu chochote.
“Kopsha, mbona umechelewa ulikuwa wapi?” aliuliza tena.
“ooooh...nilikuwa nyumbani!”
“ulikuwa unafanya nini mpaka uchelewe?”
“mimi nafikiri hawa wajumbe wote wote wapo hapa kutokana na kuambiwa kuwa kuna mkutano na sio kuhojiwa kwangu, kwa hiyo mkutano uendelee!”
“sawa ni vizuri, mkutano uendelee!” alisema mfalme akiwa amekasirika sana. Kwa siku nyingi mfalme na waziri walikuwa hawapendani kabisa. Ila mfalme alishindwa kujua ni jinsi gani ataweza kumuondoa waziri katika majukumu yake kutokana na kuwa waziri nae alikuwa na nguvu sana na karibu kila mwananchi alimpenda.
“wajumbe wote na wawakilishi wa wananchi mnaombwa usikivu ili mpate kujua ni kitu gani kilichofanya muitwe leo hii na mfalme wetu aliyetukuka!” alisema mtu wa karibu na mfalme na kuendelea
“karibu mfalme wetu mtukufu”.
Mfalme alisimama lakini hakuna mwananchi yeyote aliyempa heshima.
“kwa haraka haraka nina mambo mawili ya kuyazungumzia leo. Kabla ya yote, ndani ya ufalme wa Kopsheng tunaishi na wasaliti. Siwezi kuendelea kuona usaliti huu unatawala na kutapakaa miongoni mwa wananchi wangu. Tesh, Shen, Benjamin, Tin na Ben wote wakamatwe hapa na wauawe mbele ya macho yenu wote, ili iwe fundisho kwa yeyote atakayejaribu kusaliti ndani ya Kopsheng!”  alisema mfalme na wale aliowataja walichukuliwa na kuletwa mbele ya wajumbe.
“nikiita jina, mutampitisha mbele ili waonekane vizuri kisha mutamchinja, mmenielewa walinzi?”
“sawa!”
“Ben!” aliita mfalme na walinzi wakamchukua Ben na kuanza kumzungusha ili wajumbe wote wapate kumuona kisha akapelekwa sehemu maalumu kwa ajili ya kusubiri muda wa kutenganishwa kichwa na kiwiliwili.
“shen!” mfalme alilitaja hilo jina nae alifanyiwa kama alivyofanyiwa mwenzake na kisha kwenda kuungana na mwenzake ili kusubiri muda wao wa kunyongwa kwa kutenganishwa kichwa na kiwiliwili.
”Tin!”
“Benjamin!”
“Tesh!”
“huyo hayupo hapa mtukufu mfalme!” walinzi walijibu.
“kwa nini hamkumtafuta?” mfalme aliuliza kwa ukali.
“samahani mtukufu mfalme wetu, tulichelewa kupata taarifa mapema ya majina yao!”
“Tesh ni nani?”
“Tesh ni rafiki wa karibu wa Tosh, mtukufu mfalme wetu!”
“na huyo Tosh ni nani?”
“Tosh ni mtu wa karibu wa waziri Kopsha!”
“waziri Kopsha!?” mfalme aliuliza akijifanya kushangaa.
“ndio mtukufu mfalme!”
“waziri, kuna kitu gani kilichojificha hapa?”
”kujifichaje?” aliuliza waziri Kopsha.
“inawezekana wewe unaficha wahalifu!”
“kwa nini nifiche wahalifu wakati najua dawa ya wahalifu ni kitu gani!”
“unajua nini kuhusiana na Tesh?”
“hakuna chochote ninachokifahamu!”
“na kipi unachokifahamu juu ya Tosh?”
“Tosh ni mwananchi ambaye ninamtumia katika mambo yangu binafsi!”
“mambo binafsi?!, mambo gani hayo?, ya kuupindua na kuchukua kinguvu utawala wangu? Hahahahahahahah!” alisema mfalme huku akiwa anacheka kwa kejeli.
“mambo yangu hayahusiani kabisa na uhalifu wala uhaini, Tosh ninamtumia wakati nipo sehemu kama hii, yeye huwa yupo nyumbani kwangu ili kurekebisha na kuiweka nyumba katika hali ya usafi!”
“kwa hiyo Tosh kwa sasa yupo nyumbani kwako?”
Je nini kitatokea…
Usikose sehemu inayofuata.

JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         - SABA
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

Yule mzee alipita nyuma ya nyumba yake ambako kulikuwa na bustani ya kuvutia. Tulifika katika bustani hii na kukaa hapo. Nyumba ya huyu mzee ilikuwa ya kawaida sana, kwa muonekano wa nje. Tukiwa pale bustanini, Yule mzee aliingia ndani na kurudi na matunda ambayo nilikuwa ninayafahamu kabisa. Kulikuwa na matufaha, makongomanga, mapeasi, mananasi na matunda mengine mengi. Kilikuwa kilichosheheni matunda mengi sana.
“kuleni haya matunda!” alisema Yule mzee mara baada ya kutuletea kile kikapu.
“wewe je, hauli?” tulimuuliza.
“muda wa kula bado, kwa mwezi tunakula mara moja tu!”

Endelea…

“heeee, mwezi! Si mtakufa kwa njaa?” aliuliza Shebby.
“huko duniani kwenu ni tofauti na huku.na mimi ni tofauti na wewe!” alijibu.
“haya mazingira, hakuna jua, hakuna mwezi hizo siku mnazihesabu vipi?” aliuliza Aziza.
“mimi ni mkazi wa huku pia kumbuka kuwa mimi sio binadamu kama unavyoniona wewe. Pia nina uwezo wa kufanya jambo linaloweza kukushangaza wewe, mfano angalia hii.....!” alisema Yule mzee huku akichukua tufaha moja ambalo baadae lilioza na funza walianza kutoka katika lile tunda. Baadae alichukua wale funza na kuwaweka mkononi kish kuwatupa chini na wakageuka kuwa mkate.
“vipi unaweza kula huu mkate?” aliuliza
“ aaaaaah wewe hapana!” tulijibu huku tukijizuia kutapika.
“kuna mwenye swali?” aliuliza.
“ndio!” alijibu Aziza.
“enhe!”
“mzee itachukua muda gani mpaka pale tutakapopata msaada wa kurudi nyumbani salama?”
“jambo zuri kwa muda huu ni kuhakikisha kuwa munakuwa salama kwa kipindi chote mtakachokuwa mpo huku. Kuhusu suala la lini au kwa kipindi gani mtafanikiwa kurudi ni juhudi na kujitambua kwenu tu!” alijibu.
“kujitambua na juhudi kivipi, hatujakuelewa babu!” Shebby aliuliza.
“kujitambua na juhudi, yaani pale mtakapokuwa tayari kurejea kwenu tu, mtarejea!”
“sisi tupo tayari!”
“ndio mpo tayari ila hamjajitambua kama mpo tayari na wala hakuna juhudi mlizozionyesha kuhusu kuwa tayari”
“dah, mzee hatujaelewa kabisa!”
“usijali, bado siku kadhaa tu mtakuja kuelewa!” alisema yule mzee na kuendelea
“kuna swali jengine?”
“ndio, mimi hapa ninalo!” nilijibu
“uliza!”
“mimi nina maswali kama manne hivi!”
“sawa, uliza moja moja!” alisema.
“hili ni eneo gani?”
“ni eneo tunaloishi sisi!”
“mwanzo ulisema kuwa, watu maalumu ndio wanaopaswa kuja huku, ni wepi hao hatu maalumu?”  niliuliza.
“watu maalumu ni binadamu ambao wanajulikana sana kwa maarufu walio nao utokanao na kile wanachokifanya kama msanii, mfanya kazi, mfanya biashara na kadhalika!”
“na mualiko maalumu ni mualiko wa aina gani?”
“unaonekana mdadisi sana wewe, mambo mmengine yatakuletea matatizo matatizo sana hapo baadae, ila sawa mwaliko maalumu ni mualiko ambao aina binadamu niliokutajia huupata mara baada ya kuuomba na kusubiria majibu yao kwa kipindi kisichozidi mwezi mmoja!”
“swali langu la misho, pia ulisema kazi maalumu, je kazi maalumu ifanyikayo huku ni kazi gani?”
“kama ningejua kuwa maswali yako yanahusiana na vitu hivyo ulivyoniuliza, ningekuambia uniulize yote kwa mara moja” alisema na kumeza funda moja la mate na kuendelea
“Jambo ninalotaka mufahamu kwanza ni kuwa dunia yenu ina watu wachache wema ila wengi wao ni watu wabaya. Miaka kadhaa iliyopita eneo hili lilikuwa ni eneo ambalo lilikuwa likitoa msaada katika sayari mbalimbali ikiwemo na dunia yenu. Kama mtakumbuka au sijui kama mlishawahi kusikia kama matukio ya ajabu ajabu yanayotokea katika dunia yenu katika siku za hivi karibuni kama zamani yalikuwepo. Kwa siku za hivi karibuni, nguvu  zitokazo katika eneo hili zinatumika kwa njia isiyofaa. Hasa ni baada ya kiongozi huyu anayeongoza kwa sasa kuchukua madaraka kwa nguvu kutoka kwa mfalme ambaye alikuwa hapendelei upuuzi kama huu unaoendelea. Siku hizi eneo hili limekuwa ni eneo la kumwaga damu za viumbe wasio na hatia tu. Watu wengi huja huku kwa tamaa ya kupata mali, umaarufu au kupandishwa cheo kazini. Kwa mfano, anakuja anayejiita mwanasayansi anapewa vimelea vya ugonjwa ambao duniani kwenu haupo, kwa kutumia wadudu na wanyama kama nzi, mbu au hata popo ama mbwa wanaeneza ugonjwa huo kwa binadamu. Wanaacha kwanza uue watu kadhaa ndipo hujitokeza na kusema wanafanya uchunguzi juu ya kupata dawa ama chanjo yake kumbe tayari dawa yake wanakuwa wanayo tangu kabla ugonjwa haujaenezwa. Baadae huisambaza dawa na kupata fedha nyingi, kutokan na kutokujua kwenu munawapongeza na kuwaona wameokoa maisha ya binadamu kumbe munawapongeza wauaji. Sasa kazi maalumu ambayo huja kufanywa huku na hao watu ni kuwatoa sadaka binadamu wenzao kama malipo ya kile wanachopatia. Mfano kama mtu anamiliki magari hasa ya abiria, huja huku kwa huyu mfalme na kuchagua ni gari gani anataka kafara ya damu itoke. Ndipo unapoona gari limepata ajali harafu watu wamefariki. Huku kuna viumbe ambao wamepangiwa kazi yao ni kusababisha ajali tu. Hao wana uwezo wa kumfanya dereva asinzie wakati anaendesha kwa mwendo wa kasi au kumfanya mtu anywe pombe kupita kiasi harafu akaendesha chombo cha moto. Wengine kazi yao ni kuwatoa viumbe nakala. Pale ajali inapotokea huja huyo kiumbe ambaye humtoa mtu nakala, yaani huwa watu wawili waliofanana kila kitu. Baada ya hapo huja wengine ambao kazi yao kubwa ni kuwachukua wale waliokuwa watu haswa ambao kiukweli huwa wameumia kidogo na kuondoka nao, huwa hawajafa kwa sababu mungu pekee ndiye mwenye amri ya kuchukua roho ya kiumbe wake. Zile nakala huachwa katika eneo la ajali na pindi wanapokuja madaktari husema wale watu wamefariki. Inabidi lazima zile nakala zife kwa sababu kwa sababu mtu mmoja hatakiwi kuishi kwenye nafsi mbili tofauti. Wale watu wakishaletwa huku hutolewa kiasi kidogo cha damu na kasha hutumikishwa kwa hiyo kazi maalumu wanayokuja kuifanya huku ni kupata mali, umaarufu, na pia kutoa sadaka ya binadamu. Ila naomba mtambue kuwa sio kila unayemuona ana mafanikio, ana mali nyingi au maarufu sana sio kama amepatia huku mafanikio, la hasha! Wengine ni bidii na juhudi zao ndizo zilizowafanya wafanikiwe!” alimaliza na kutufanya tujenge taswira na kuanza kuwafikiria watu maalufu wengine wakipata umaarufu kwa vitu vya kipuuzi.
“huyo kiongozi wa zamani yupo hai au ameshakufa?” niliuliza
Ýupo hai mpaka leo, uzuri wake ni kuwa ni kuwa hakuna kati ya viumbe wabaya wenye kujua pale alipo, ila kila siku wanaishi naelakini hawamjui. Kila siku wanamtafuta kwa udi na uvumba kwa kujua kuwa kuna sehemu alipojificha!” alijibu.
“wewe unamjua?” Shebby aliuliza. Yule mzee alimuangalia Shebby kwa makini kwa sekunde kadhaa.

Je atajibu nini, usikose sehemu inayofuata.

JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         - SITA
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

“wale ni wapelelezi na wale waliokuwa na rangi nyeusi na kijivu askari kwa ajili ya mauaji. Inavyoonekana taarifa za kuja kwenu hapa zimeshajulikana. Wale wana uwezo wa kujua wanaomtafuta yupo wapi au ameelekea wapi. Pale wameshindwa kujua upande mlioelekea kwa sababu ya hiyo fimbo. Hiyo fimbo ni msaada mkubwa kama itatumika ipasavyo. Hiyo sio fimbo kama munavyoiona. Hiyo ni dagger maalumu yenye uwezo wa kuua mashetani ya kijini na kibinadamu pia. Wote walioshindikana kutokana na uhalifu wao, hapo ndio mwisho wao. Inafanya kazi kutokana na fikra za mtu aliyeichukua. Ina uwezo wa kubadilika na kuwa silaha yeyote kulingana na matumizi ya wakati husika” alisema.
“Dagger ndio nini?” shebby aliuliza 

Endelea…
“dagger ni lugha tu ya kigeni, maana yake ni visu vidogo vyenye ncha kali vinavyotumika katika mapambano ya karibu au close combat kwa lugha nyengine. Ila kwa huku kwetu dagger ni visu maalumu vilivyonakshiwa na kupambwa na lugha za kijini. Mara nyingi vilitumika katika kuwaangamiza viumbe ambao sio wa kawaida. Visu hivi vilikuwa vinatumika miaka mingi iliyopita katika falme ya uajemi katika dunia yenu na chimbuko lake ni huku. Vilitolewa kwa ajili ya kuleta amani miongoni mwa falme ingawa wengine walikuja kutumia vibaya na kusababisha machafuko ambayo yanaendelea mpaka leo. Tofauti na visu vyengine, visu hivi huwa na rangi ya dhahabu na vito viwili katika mpini wake. Upande mmoja huwa na kito cha rangi ya kijani na upande wa pili kito cha rangi nyekundu” alisema. Wakati huo bado tulikuwa tukimfuata yule mzee kwa njia ya mstaari. Nilijaribu kuiangalia vizuri ile fimbo na ndani ya zile nakshi, ulionekana kitu mithili ya kimiminika cha rangi ya dhahabu ambacho kilikuwa kinatembea tembea. Wakati nikiendelea kuangalia kwa makini, nilistuka baada ya ile fimbo kujichora herufi “A” na baadae kujichora maandishi ambayo nilikuwa siyafahamu. Niliogopa sana.
“mzee, angalia hii ni nini sasa?” nilimuuliza huku nikimuonyesha ile fimbo. Mzee alikataa kuishika ile fimbo.
“inaonekana una bahati sana!” alisema na kuendelea
“kuanzia leo hiyo fimbo utakuwa nayo siku zote za maisha yako. Hiyo inaonyesha kuwa wewe utakuja kupata matatizo sana hapo baadae, kwa hiyo fimbo imekuchagua wewe kuambatana nayo mpaka pale matatizo yatakapokwisha” alisema.
“mbona sielewi mimi?” nilimuambia.
“utakuja kuelewa tu, kuna kitu unamfanyia mjomba wako kwa hiyo lazima kuna jambo baya litakuja kukutokea , pia naona una mpenzi huku huku!” alisema huku akiendelea kucheka.
“.....ila tuyaache hayo, la umuhimu ni kuwasaidia kuweza kurudi duniani salama..!” alisema.kila mmoja alishangaa juu ya matukio yaliyokuwa yakiendelea huku.
“karibuni nyumbani kwangu, tumeshafika!” alisema baada ya kutumia dakika thelathini na saba tangu pale tulipokutana nae mpaka kufika pale alipokuwa anasema ni nyumbani kwake.
“nyumbani kwako?” tulimuuliza huku tukistaajabu kwa sababu hakukuwa na dalili zozote za uwepo wa makazi ya watu katika maeneo hayo, bado kulikuwa kunaonekana kuwepo kwa jangwa tu.
“ndio, hapa ndipo ninapokaa” alijibu huku akituamuru tumsubirie tumsubirie oale mpaka atakaporudi.
“hamruhusiwi kusogea hata hatua moja!” alisema huku akianza kuondoka. Tulimuangalia akiwa anatembea kwa takribani mita saba tokea pale alipotuacha kisha akapotea. Hali ile ilitufanya tustuke sana mpaka Tina akakimbia toka pale tulipokuwa tumekaa. Sekunde mbili tu tangu alipokimbia,ghafla alianguka chini. Pale pale aliumia vibaya kwenye mguu. Tulimchukua na kwenda nae pale alipotuacha yule mzee.
“ndo umefanya nini tena Tina?” aliuliza Hamza. Lakini Tina hakuwa na jibu badala yake alikuwa akiugulia maumivu.
“hampaswi kuogopa, lazima tushikamane na kuwa majasiri!” alisema Shebby.
“kweli kabisa, kwa sababu hata tukisema tukimbie, tutakimbilia wapi, huku kote hakuna hata mmoja kati yetu mwenye kupajua hapa!” alichangia Aziza.
“ni kweli, unaweza kkukimbia hapa harafu ukaenda kukamatwa na watu wa kiongozi wao. Itakuwa umefanya nini sasa, kama huyu mzee angekuwa ni mtu mbaya wala tusingefanikiwa kufika kufikia katika eneo hili angetuacha tuangamizwe na wale viumbe!” nilisema
“swadakta!” alichangia Hamza na Aziza.
Tulikaa pale tukimsubiria yule mzee. Baadae alikuja akiwa ameshika chupa ndogo ndogo tano kulingana na idadi yetu zenye maji maji ya rangi ya zambarau. Alitugawia kila mmoja chupa moja na kutuamuru tunywe akisema ni dawa ya kujitambua.
“mtakapokunywa hii dawa, wale wenye kuwafuatilia hawatoweza tena kujua mahali mlipo hivyo kutawafanya kuwa salama zaidi mpaka pale suala la kurudi kwenu duniani litakapokamilika!” alisema kwa msisitizo
Hakukuwa na majadiliano zaidi kuhusu suala  la kunywa zile dawa. Kila mmoja alitaka abaki akiwa salama kabisa npaka pale suala la kusaidiwa kurudi duniani litakapokamilika. Kila mmoja alichukua chupa yake na kuanza kuinywa. Mara baada ya kunywa ile dawa, taratibu nguvu zilianza kuniishiana baadae nuru ilianza kupotea machoni kwangu. Baadae ilitoweka kabisa na kujikuta sijitambui. Sijui ni kwa muda gani nililala pale chini, ila baadae nilikuja kuzinduka na kukuta mazingira yamebadilika sana. Niliwaangalia wenzangu, Aziza alikuwa tayari ameshaamka kabla yangu. Hamza na Tina ndo walikuwa wanaanza kuzinduka kutoka katika ule usingizi. Baada ya dakika moja, Shebby nae akaamka. Nilipoangaza vizuri pembeni, ile fimbo sikuiona, badala yake kulikuwa na kisu chenye urefu wa sentimita kama ishirini hivi. Kilikuwa kimenakshiwa na dhahabu tupu katika mpini huku kukiwa na maandishi ambayo sikuweza kuelewa yalikuwa ni ya lugha gani. Pia katika mpini kulikuwa na kitu chenye umbo la duara chenye kung’aa sana. Upande mmoja kilikuwa cha rangi ya kijani na upande mwengine kilikuwa cha rangi nyekundu. Kwenye makali yake, kulikuwa na maandishi yaliyokuwa yanatoa nuru ya ajabu. Niliinuka toka pale chini na kuangaza huku na huko. Kulikuwa na miti michache, nyumba na nyasi lakini vyote vilikuwa na rangi moja tu, nyeupe. Nilijaribu kuangalia juu, hakukuwa na mawingu wala jua wala mwezi. Mwanga wa kawaida tu ambao chanzo chake sikupata kukifahamu ndio uliokuwepo katika eneo hili. Yule mzee alikuja pale tulipokuwa tumekaa.
“habari zenu!” alitusalimia.
“salama!”
“nyie mnalala sana!” alisema
“ni kwa kipindi gani tulikuwa tumelala?” Hamza aliuliza.
“ni wiki mbili sasa!”
“aaah, wiki mbili tupo hapa hapa tu, hahahaha hilo haliwezekani kabisa!” alisema Shebby.
“ndo hivyo wiki mbili, mlikuwa mmelala haha nje, nilikuwa nawageuza geuza tu hapa kama samaki wanaokaangwa!”
“duh, sasa si tungekufa kwa njaa, siku zote hizo!” nilisema.
“kikubwa sasa hivi, karibuni ndani!” alisema na kuanza kuondoka pale, tulimfuata.
Yule mzee alipita nyuma ya nyumba yake ambako kulikuwa na bustani ya kuvutia. Tulifika katika bustani hii na kukaa hapo. Nyumba ya huyu mzee ilikuwa ya kawaida sana, kwa muonekano wa nje. Tukiwa pale bustanini, Yule mzee aliingia ndani na kurudi na matunda ambayo nilikuwa ninayafahamu kabisa. Kulikuwa na matufaha, makongomanga, mapeasi, mananasi na matunda mengine mengi. Kilikuwa kilichosheheni matunda mengi sana.
“kuleni haya matunda!” alisema Yule mzee mara baada ya kutuletea kile kikapu.
“wewe je, hauli?” tulimuuliza.
“muda wa kula bado, kwa mwezi tunakula mara moja tu!”
Itaendelea…

JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         - TANO
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

“tusipoangalia hapa, tutashindwa vibaya sana kwa siku zijazo, hilo ni kutokana na kushindwa kupatikana kwa kito chenye rangi ya bluu kilichopo katika kisiwa kimoja katika dunia” alisema mfalme
“nimekuelewa kiogozi wangu mtukufu!”alijibu Edmund.
“je kuna taarifa nyengine ya ziada?” aliulliza mfalme
“ndio kiongozi, kuna Magreth Kimario na Lawrence Majoka walitaka kuja huku ili kukamilisha kafara zao juu ya mahitaji yao kama walivyoahidi, wanasubiria ruhusa yako tu” alisema Eldon.
“Edmund taarifa hizi ni za kweli?” mfalme aliuliza.

Endelea…

“ndio mfalme!”
“sasa wape taarifa kuwa tutakutana katika kikao chetu kitakachofanyika siku zijazo huko huko duniani. Kwa sasa lazima tule sahani moja na maadui zetu wanaojitokeza. Nataka mpaka kesho niwe tayari nimeshapata taarifa zote kuhusu wale wasaliti ambao nimewatambua, wengine lazima muwafuatilie kwa umakini wa hali ya juu sana, hata Kopsha pia simuamini kwa sasa, ila ufuatiliaji wa Kopsha unahitaji akili na ustadi wa hali ya juu, musifanye makosa hata kidogo, mkikosea tu, itatugharimu sisi sote!” alisema mfalme
“sawa mfalme”
“haya, watu wote wa baraza twendeni katika ukumbi wa kifalme, Jackson tutaonana wakati mwengine, nenda ukafanye shughuli nyengine, kikao kimeisha kwa leo”alisema mfalme na kutoka katika kile chumba cha siri na baadhi ya washirika wake ambao walikuwa ni watiifu kwake. Edmund Jackson alitoweka tu ghafla kwa maajabu.
                                                  *******************************************************
Tulibaki vinywa wazi tukistaajabu na kujiuliza maswali mengi kuhusu majibu aliyokuwa ameyatoa Shebby. Kwa nini alijifanya hapajui kumbe anapajua hapa, alikuwa ana nia gani kwetu.tulijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu ya uhakika.
“ulishawahi kufika hapa?” yule mzee alimuuliza Shebby. Wote tulikuwa makini kuyasikiliza majibu ya Shebby.
“hapana, sijawahi kufika katika eneo hili hata mara moja katika maisha yangu!” alijibu Shebby.
“ulipajuaje hapa?”
“kwa kusoma vitabu, mimi ni mpenzi mkubwa wa kusoma vitabu na pia kusoma vitabu vya mitandaoni. Kuna siku moja niliwahi kusoma kitabu kilichokuwa kinaelezea uwepo wa nchi ambayo mazingira yake ni tofauti kabisa na mazingira tuliyoyazoea sisi, kwa jinsi mazingira yake yalivyo unaweza kufananisha na mazingira yanayopatikana katika katika bara la Antarctica lenye kutawaliwa na barafu kila upande lakini maajabu ya maeneo haya ni kuwa hakuna baridi kama inayopatikana ndani ya Antarctica. Kwa hali nisiyoitegemea leo nimekuja kuiona mwenyewe” alisema Shebby.
“Bara la Antarctica ndio kitu gani?” aliuliza yule mzee.
“ni moja kati ya sehemu ya nchi kavu kule duniani. Kutokana na hali ya hewa iliyopo, binadamu ni nadra sana kuishi huko. Eneo hilo lipo katika kizio cha kusini cha dunia. Kwa kifupi hakuna makazi ya binadamu yanayopatikana huko!” nilijibu kwa kifupi.
“sawa, vizuri, sasa ngoja niwaambie, yaani mumefanya makosa makubwa sana kufika katika eneo hili. Sio watu nyinyi munaohitajika kuja katika eneo hili. Na mpaka sasa hivi nafikiri kiongozi wa eneo hili tayari atakuwa ameshajua ujio wenu huku, kwa hiyo sijui hata niwasaidieje!” alisema yule mzee.
“mzee wetu, tunaomba utusaidie” alisema Hamza.
“sijui niwasaidie vipi!”
“tafadhali mzee wetu, tungefurahi sana kama ungeweza kutusaidia kupata kurejea nyumbani”
“anhaaa, kwa hilo nitajaribu!”
“samahani mzee naomba kuuliza!” nilisema.
“enhe!”
“mzee kwani hii ni sehemu gani mpaka utuambie sisi hatukupaswa kuja katika eneo hili?”
“wewe ulidhamiria kuja hapa?” alinijibu kwa swali badala ya jibu.
“hapana!”
“unalijua eneo hili?”
“hapana”
“na ndio maana nakuambia haikupaswa nyie kuja katika eneo hili!” alisema kwa msisitizo.
“kwa nini?”
“usiulize maswali mengi, kwani kikubwa ukitakacho ni kitu gani?”
“msaada!”
“sasa subiri kwanza nijaribu kuwapatia msaada mnaouhitaji ila kwa kukusaidia ni kuwa nyie hamkuwa binadamu mnaopaswa kuja huku. Huku huja binadamu maalumu kwa kazi maalumu, kwa mualiko maalumu na kwa wakati maalumu!”
“Binadamu, kazi, mualiko na kazi maalumu?
“ndio, nafikiri umenisikia vizuri!”
“binadamu maalumu ni binadamu wa aina hani hao?”
“binadamu...binadamu sio muda wa maswali na majibu sasa hivi. Mtaniuliza tukifika nyumbani kwangu. Hapa mkikutwa, mtauawa, tuondoke hapa haraka!” alisema yule mzee
“sawa” tulimjibu.”
“chukua hii!” alisema huyu mzee na kutoa fimbo moja yenye rangi nyeupe iliyokuwa inang”aa sana. Pia fimbo ile ilikuwa imenakshiwa kwa kutumia rangi ile ile nyeupe. Ilikuwa na urefu wa sentimita thelathini hivi. Kila mmoja alikuwa anakwepa kuichukua ile fimbo.
“kama mnataka msaada, nimewaambia munisaidie kuibeba hii fimbo, harafu mtanifuata!” alisema yule mzee. aliiacha ile fimbo chini na taratibu akaanza kuondoka. Tulishauriana na wenzangu, kisha niliamua kuichukua ile fimbo na tukamkimbilia yule mzee.
“kitu gani munachokiona?” aliuliza yule mzee mara baada ya kumfikia.
“hakuna kitu tunachokiona zaidi ya jangwa tu!”
“sawa, sasa lazima mpite mule ninamopita mimi, tumeelewana?
“sawa mzee”
“nani aliyeichukua ile fimbo?”
“mimi!” nilijibu.
“masharti ya hiyo fimbo ni kuwa pindi uichukuapo hautakiwi kuiacha kamwe. Na nataka muone faida ya hiyo fimbo, nyoosha kuelekea kule mlikotoka harafu muangalie vizuri”
Nilinyoosha ile fimbo kwa kufuata maelekezo ya yule mzee. Tulikuwa tumeshatembea kwa takribani mita mia tatu hivi. Baada ya kunyoosha, pale tulipokuwa tumesimama kuongea na huyu mzee, tulipata kuwaona viume ambao sikupata kuwafahamu mara moja. Walikuwa wakizunguka zunguka katika eneo lile. Walikaa pale kwa muda kisha wakaondoka kuelekea katika eneo jengin tofauti na upande tuliokuwa tupo sisi.
“mmewaona wale viumbe?” aliuliza yule mzee.
“ndio!”
“munajua pale walikuwa wakifanya nini?”
“hapana!”
“wale ni wapelelezi na wale waliokuwa na rangi nyeusi na kijivu askari kwa ajili ya mauaji. Inavyoonekana taarifa za kuja kwenu hapa zimeshajulikana. Wale wana uwezo wa kujua wanaomtafuta yupo wapi au ameelekea wapi. Pale wameshindwa kujua upande mlioelekea kwa sababu ya hiyo fimbo. Hiyo fimbo ni msaada mkubwa kama itatumika ipasavyo. Hiyo sio fimbo kama munavyoiona. Hiyo ni dagger maalumu yenye uwezo wa kuua mashetani ya kijini na kibinadamu pia. Wote walioshindikana kutokana na uhalifu wao, hapo ndio mwisho wao. Inafanya kazi kutokana na fikra za mtu aliyeichukua. Ina uwezo wa kubadilika na kuwa silaha yeyote kulingana na matumizi ya wakati husika” alisema.
“Dagger ndio nini?” shebby aliuliza 

Je atamjibu kitu gani, usikose sehemu inayofuata.


JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         - NNE
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

“haujui?, hebu elezea ilikuwaje ukawa katika sehemu hii, yaani tukio la mwasho kulikumbuka?”
“ahnha ni..ni...nili...nilikuwa natoka nyumbani ili kuelekea kwa rafiki yangu ghafla nikiwa njiani nikahisi kuishiwa nguvu harafu kuna upepo nikahisi ulikukwa unavuma sana. Ulikuwa ni upepo mkali sana hali iliyonifanya kufumba macho ili mchanga usije ukaingia machoni. Nilishindwa kukimbia kutokana na kuishiwa nguvu. Baada ya dakika kadhaa nguvu zilirudi na ule upepo ulikuwa umeisha. Nilipokuja kufungua macho, nilistaajabu kwa sababu sikuwepo pale, nilikuwa katika sehemu nyengine, sehemu yenye mazingira ambayo siyafahamu, ni mazingira haya katika sehemu hii!” alimaliza hamza. Ilikuwa ni hadithi ya kustaajabisha kidogo.

Endelea…

“oooooh! Kumbe, enhe na wewe unaitwa nani?” aliuliza tena yule mzee.
“Tina!”
“Tina, unapajua huko ulikotoka?”
“hapana sipajui”
“enhe na hapa ulipo unapafahamu?”
“hapana!”
“na wewe ilikuwaje ukawa katika eneo hili ambalo haulifahamu?”
“nikiwa natoka kwa shangazi ambako niliagizwa na mama, ilibidi nivuke barabara ili nipate kurejea nyumbani. Niliangalia kulia na kushoto bila ya kuona gari yeyote inayokuja. Nikiwa katikati ya barabara, ghafla nilijikuta nimerushwa juu nikadondoka chini. Pale pale watu walijaa na niliwasikia tu wakisema tumpeleke hospitali, mara wengine wakisema nimeshaaga dunia tayari. Taratibu nuru ilipotea machoni kwangu na baadae nikalala kabisa. Nilipokuja kuamka ndio nikajikuta nipo katika eneo hili.”
“mh! Na wewe unaitwa  nani?”
“Aziza!”
“ilikuaje ukawa katika sehemu ambayo hauifahamu?”
“mimi?”
“Ndio wewe, au unapajua hapa?”
“hapana!”
“enhe ilikuwaje sasa?”
Aziza nae akaeleza jinsi ambavyo alifika pale.
“Sawa!” alisema yule mzee mara baada ya Aziza kumaliza kuhadithia njia illiyomfanya kufika pale.
“wewe unaitwa nani?” aliuliza yule mzee huku akiniangalia mimi. Sikujibu kitu bali nikageukia pembeni tu.
“nakuuliza wewe hapo!” alisema yule mzee huku akinishika begani.
“sijajua ni imani kiasi gani niliyonayo kwako mpaka nikutajie jina langu, kama sipati msaada mpaka nikutajie jina langu, basi” nilijibu lakini nikiwa na woga sana.
“hakuna kitu chenye kufichika huku, hauwezi kunificha kitu kabisa, wewe unaitwa nani?”alisema yule mzee na kuonyeshea kidole mwanaume mwengine.
“shebby!”
“Shebby?”
“ndio!”
“na wewe kwako ilikuwaje ukafika hapa, au unapajua hapa?”
“ndio napajua!” alijibu Shebby hali iliyofanya wote tustuke na kubaki tukishangaa kile alichokijibu Shebby. Ina maana muda wote tuliokuwa tunasumbuka kutafuta msaada, kumbe shebby alikuwa anapafahamu huku tulipo.
Tuliona huyu anaweza kuwa ni mtu mbaya kwetu. Uaminifu juu yake ukapotea.
                                   *************************************************************
Ni katika makao makuu ya Kopsheng, mfalme alionekana katika chumba chake cha siri akiwa na baadhi ya wasaidizi wake muhimu.
“nipeni taarifa, ni kitu gani kinachoendelea kusikika miongoni mwa wananchi wangu?” aliuliza mfalme.
“mtukufu mfalme, kutokana na tetesi zinazoongelewa na walio miongoni mwa wananchi wako ni kuhusu suala la utawala wako. Ila kubwa na lililonistua ni tetesi za kuupindua utawala wako, hilo ndilo kubwa na hayo ndio yaliyonifikia kutoka kwa wapelelezi wetu walio katika kila kona ya ufalme wako. Alijibu mmoja wa washirika.
“sawa, kazi nzuri Eldon, kwa hiyo hawa wananchi bado wana mipango ya kuupindua ufalme wangu kweli, nawashangaa tu, hawa ni viumbe gani wasiokata tamaa, kila atakayejaribu nitampeleka kule anakostahiki, kuzimu!” alisema mfalme.
“kitu kingine ninachohisi ni kuwa, nyuma ya hawa wananchi wapo viongozi ambao muda wote tupo nao muda wote katika shughuli zote za kifalme” alisema Eldon.
“Eldon, kwa kutumia uwezo wako mkubwa wa miujiza ulionao, bado tu haujapata kuwajua hao walio nyuma ya wananchi ambao wana mpango wa kuubomoa ufalme wangu?” aliuliza mfalme.
“hapana kiongozi, inaonekana hao walio nyuma ya wananchi wana uwezo mkubwa sana kuliko ule niliokuwa nao mimi!” alisema Eldon.
“hebu subiri kwanza niangalie huyo fukunyuku ni akina nani!” alisema mfalme na kufumba macho yakehuku akiwa ameibana miguu yake kwa nguvu kama mtu anayeizuia haja ndogo isitoke. Ilimchukua dakika tatu kuwa katika hali hiyo. Alifumbua macho na kisha kuwaangalia wasaidizi wake mmoja baada ya mwengine.
“wapo waasi kumi na moja, ila kuna watano nimeshindwa kuwatambua. Niliowatambua ni Tesh, Shen, Wesh, Tin, benjamini na Intiswari, sasa hawa munajua ni kitu gani cha kufanya juu yao. Sasa ili kuweza kuwatambua wengine ambao nimeshindwa kuwatambua, nipeni majina ya wapiganaji wenye uwezo mkubwa ndani ya ufalme wa Kopsheng wanaoitwa mashujaa. Nafikiri hao ndio wanaweza kuwa miongoni mwa hawa watano ambao sijawafahamu” alisema mfalme.
“aaah mtukufu mfalme wangu, hao ni waziri Kopsha, kuna mtu wake wa karibu anaitwa Tosh, mwanawe waziri Kopsha anayeitwa Tush, wengine ni Angel, Samson, mfalme aliyepita anayeitwa Cysery pamoja na mmoja hivi ambaye sifahamu jina lake halisi ila jina la utani anaitwa Black bird. Pia kuna wengine kama wanne hivi majina yao siyafahamu mtukufu mfalme” alisema Eldon
“kuanzia sasa amuru wapelelezi wetu kuwafuatilia kwa ukaribu zaidi hao wasaliti, hasa Kopsha, umenielewa Edmund, na Eldon atakuwa ndiye kiongozi wao” alisema mfalme.
“ndio mtukufu wangu, hilo halina shida, ila Invy amesema ana taarifa ambayo itakuwa ni ya kustusha sana, kwa heshima yako namuomba atoe hiyo taarifa” alisema Edmund Jackson huku akimuangalia mfalme ambaye alitoa ruhusa kwa ishara ya kunyoosha mkono.
“mtukufu mfalme, kupitia kwa wapelelezi ninaowaongoza mimi, tumegundua uwepo wa binadamu ambao wamekuja kwa njia isiyo  rasmi, kutokana na ratiba niliyoipata toka kwa anayeratibu safari na mialiko yote tunayowapatia, amesema hakuna ratiba yeyote ya safari ya binadamu yeyote aliyepangiwa kuja huku kwa muda huu” alisema Invy.
“usiwe na shaka sana juu ya suala hilo Invy. Mmoja kati ya hao watu ni mtumishi wetu anayeitwa Alfonse  Daniel, nafikiri wengi wenu munamtambua. Kwa hiyo yeye atatuletea taarifa zote kama ujio wa watu hao ni wa kheri au ni wa shari.
“lakini mtukufu, kutokana na taarifa za awali zinasema kuwa watu hao hakuna hata mmoja aliyekuwa amedhamiria kuja huku.sasa hapa ndio kwenye mkanganyiko, kama hawajapanga huku kuna mambo mawili, la kwanza wamekuja kwa bahati mbaya labda walitolewa kafara ila haijakamilika ndo wamekuwa ni wazururaji huku, au pili inawezekana kuna mmoja wa wananchi amewaleta huku, ila kwa nini waletwe wakati huu, hapo ndipo wasi wasi wangu unapoongezeka!” alisema Edmund kwa msisitizo
“wewe taarifa za kuwa watu hao wamekuja hapa pasi na kukusudia umezipata wapi? Aliuliza mfalme.
“kiongozi umesahau kuwa mimi ndiye msaidizi wako?, taarifa juu ya ujio wa hao binadamu nilipozipata toka kwa Alfonse Daniel tu, nilifanya uchunguzi na kuyagundua hayo. Ni jukumu langu kuhakikisha himaya yako inakuwa salama siku zote mtukufu mfalme wangu!” alisema Edmund.
“sawa vizuri sana” alisema mfalme huku akimpigapiga Edmund begani.
“tusipoangalia hapa, tutashindwa vibaya sana kwa siku zijazo, hilo ni kutokana na kushindwa kupatikana kwa kito chenye rangi ya bluu kilichopo katika kisiwa kimoja katika dunia” alisema mfalme
“nimekuelewa kiogozi wangu mtukufu!”alijibu Edmund.
“je kuna taarifa nyengine ya ziada?” aliulliza mfalme
“ndio kiongozi, kuna Magreth Kimario na Lawrence Majoka walitaka kuja huku ili kukamilisha kafara zao juu ya mahitaji yao kama walivyoahidi, wanasubiria ruhusa yako tu” alisema Eldon.
“Edmund taarifa hizi ni za kweli?” mfalme aliuliza.

Je taarifa hizo ni za kweli au uongo, usikose sehemu inayofuata

JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         -TATU
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

“kiongozi wetu, sisi huwa hatukupingi mara nyingi kwani maamuzi ambayo huwa unayachukua huwa na matokeo mazuri baadae, ila swali langu ni kiumbe gani huyo ambaye umefikiria kumleta ili kutusaidia katika suala letu la kuirudisha nchi kule ilikotoka kwenye asili yetu watu wa Kopsheng?” mshirika mwengine aliuliza.
”Binadam, binadam ndio viumbe ambao nimefikiria kuwaleta ili kutusaidia kukabiliana na matatizo yanayotukabili” kiongozi alibainisha.
“binadam?!.....” aliuliza mmoja wao kwa mshangao akaendelea.

Endelea…

“hawa si ndo wale wanaokuja huku kila siku kuomba msaada na kwa tamaa yao ya kuwa maarufu, ukubwa wa cheo kazini au kupata mali si ndo wanawatoa wenzao kafara kwa ajili ya kupata damu?” 
“sio kwamba samaki akioza mmoja  wote watakuwa wameoza, hapana!...”  alijibu kiongozi na kumeza funda kubwa la mate na kisha akaendelea
“endapo utakuwa unatupa samaki wote kwenye jalala baada ya mmoja wao kuoza, jua utakuwa unakosa mambo mazuri na muhimu katika maisha. Jaribu kuchambua na wapo wazima kati yao. Mara nyingi kiumbe kinachofanya mambo ya hovyo na uasi huitwa shetani, sasa hao mashetani wapo kwa binadam na hata kwetu pia. Leo tumekutana ili kujadili jinsi ya kuichukua nchi yetu toka kwa huyu shetani. Basi jua kua katika kundi la mambo, wengine ni kenge, nafikiri mtakuwa mmenielewa?”
“nndiooo…..hhapanan..!” kila mshiriki alijibu kwa jibu lake.
“Sijajua nini ambacho hakijaeleweka, ila tusipoteze muda kwa kuanza kuulizana maswali mmoja mmoja acha mimi nirejee kufafanua. Namaanisha kuwa sio kama binadam wote ni wenye tamaa sio woteni wenye tabia mbaya, la hasha!,  wapo ambao wana tabia nzuri, wapo wenye hekima pia. Kwa hiyo  kuhusu suala hilo msijali kabisa, tumeelewana hapo?” aliuliza tena kiongozi.
“ndiooooo!” washirika wote walijibu kwa kifupi.
“sawa..sawa..sawa, sasa tatizo lililopo ni kuwa, nilipanga waje binadamu wanne ili kuleta msaada, badala yake wapo watano. Kwa hiyo inaonyesha mmoja kati yao atakuwa hayupo katika mpango wetu, atakkuwa amepandikizwa. Sasa sijajua nani atakayekuwa amemleta na pia ameletwa kwa wema au kwa ubaya. Pia hata kumfahamu binadamu mwenyewe kwangu imekuwa ni vigumu, kwa hiyo hata silaha ile sijui ni nani wa kumpatia kwa sababu nahisi mmoja kati yao atakuwa ni binadamu mbaya” alimaliza
“kwa hiyo tunafanyaje kiongozi” mmoja wa washirika aliuliza. Wote walikaa kimya bila ya kujibu chochote wakionekana mawazo mazito kutawala vichwa vyao. Baada ya kimya cha takribani dakika tatu, mmoja wa washiriki alijikohoza kidogo hali iliyofanya wote waliokuwepo pale kugeuka na kumuangalia.
“aaaaah mimi naweza kuwatambua baadhi yao ila sio wote. Kwa wale waliokusudiwa, nitaweza kuwatambua wawili ama watatu tu, na hao mmoja wapo ndio atakayekuwa na hiyo silaha.” Alisema
“aaaah ila nimekumbuka, tatizo ni dogo sana kuhusu wa kumpa silaha, mnajua silaha hakuna atakayeweza kuichukua kama hatokuwa ni mtu sahihi.” Alisema.
“ni kweli, hilo wazo nilikuwa sina kabisa!” alisema kiongozi wao na kuendelea,
“kwa hiyo hapa kwa leo mkutano wetu umefungwa, mpaka pale tutakapoona kuna umuhimu wa kujulishana jambo jengine, basi tutajulishana.” Alisema kiongozi na kufunga kikao ambapo washirika wote walitawanyika na kuendelea na mambo mengine.
                                            ********************************************************************
Nilipata kuwaona watu ambao walikuwa ni binadamu kama nilivyo mimi.nilifarijika na kujiona ni mtu mwenye bahati ya kuwapata binadamu wenzangu ambapo niliamini kwa kiasi fulani wangeweza kunipatia msaada. Walikuwa ni watu wanne, wanaume wawili na wanawake wawili. Mwanaume mmoja alikuwa na asili ya kiarabu na mwengine alikuwa na asili ya kiafrika wakati mwanamke mmoja alikuwa shombe shombe wenye mchanganyiko wa kiarabu na kisomali na mwengine akiwa na asili ya kibantu. Nilivyowaangalia, walionekana ni watu waliokuwa wakielekezana jambo. Niliamua kusogea mpaka pale walipokuwepo.
“habari zenu ndugu zangu!” niliwasalimiaingawa sikuwa na uhakika kama kuna hata mmoja kati yao aliyeijibu salamu yangu. Wote waligeuka na kuniangalia.
“samahani ndugu zangu!” niliongea na kuendelea
“ninawaombeni msaada, jina langu ni Abdam. Kwa hali ambayo siifahamu nimejikuta tu nipo hapa. Sijajua ni kwa jinsi gani nimefika hapa. Nashindwa kujua hapa ni wapi na ni njia gani itakayonifanya niweze kurudi nyumbani salama”
“enhe kwa hiyo?” aliniuliza yule mmoja ya wanaume aliyekuwa na asili ya kiafrika zaidi.
“naombeni mnisaidie, ikiwezekana nipate kujua hapa nilipo ni wapi na kama mnaweza kunipatia msaada wa kurejea nyumbani!” niliwaambia. Hakuna aliyejibu, wote walikuwa wakiniangalia tu. Baada ya dakika takribani tatu hivi, mmoja kati yao aliongea
“Aziza unapajua hapa?”
“hapana!”alijibu kwa kifupi yule msichana mwenye asili ya mcanganyiko wa kiarabu na kisomali.
“Tina je?”aliendelea kuuliza.
“hapana!”
“Hamza?”
“hapana!”alijibu yule mwanaume mwenye asili ya kiarabu.
“sisi wote hatujui hapa tulipo ni wapi na pia tunashindwa ni kwa jinsi gani tunaweza kurejea nyumbani kwetu salama!” alisema yule mwanaume.
“kwa hiyo mnafanyaje?” niliuliza.
“kufanyaje? Kwani wewe unafanyaje, si kutafuta msaada au, mbona unauliza swali la kijinga hivyo, huo ni upumbavu” alijibu yule mwanaume.
“oh!” niliguna tu, kweli nilijiona nimeuliza swali ambalo lilikuwa ni la kipuuzi.
Wale watu waliendelea kusonga mbele, nami niliamua kuungana nao kwani hakukuwa na njia iliyo bora zaidi tofauti na kuandamana nao. Niliona ni bora kufuatana nao ili kutafuta msaada tukiwa tupo wengi tofauti na kama nikiwa nipo peke yangu. Hakuna aliyemsemesha mwenzake njiani. Tulitembea tukiwa katika hali hiyo ya kutosemeshana kwa takribani dakika arobaini hivi, ndipo kwa mbali tulipopata kumuona mzee mmoja aliyeonekana amesimama akiwa na fimbo yake.tofauti na watu wote tuliokutana nao njiani, huyu mzee sura yake ilikuwa inaonekana vizuri. Tulimsogelea yule mzee kwa minajiri ya kuomba msaada kwake. Alikuwa ni mzee mwenye nywele nyeupe kabisa. Wala haikuonekana nywele nyeusi kwake. Pia alikuwa amevaa yenye rangi nyeupe yaliyokuwa yanang’aa sana. Alishika fimbo ndefu iliyompita hata kimo chake kwa takribani sentimita mbili hivi. tuliamua kumsogelea yule mzee ambaye hakuwa akijali ujio wetu kwake.
“habari yako mzee?” tulimsalimia mara baada ya kumfikia pale alipokuwa amesimama hali iliyomfanya kustuka na kutuangalia. Hakujibu kitu bali aliishia kutuangalia tu.
“habari ya muda huu mzee?” tulimsalimia tena.
“salama, habari yenu?”
“nzuri mzee wetu!”
“vipi , mnataka niwasaidie nini mbona munaniangalia hivyo?”
“samahani mzee wetu!”
“enhe!”
“tunaomba msaada wako, tunaomba utusaidie!”
“msaada gani munaouhitaji tokea kwangu?”
“kama itawezekana tujue ni kwa jinsi gani tutaweza kurudi nyumbani!”
“msinishangaze bwana, kwani huko mlikotoka ni wapi?”
“hatujui!”
“kama hamjui mlikotoka, sasa hapa mlifikaje?”
“hatujui mzee wetu”
“wewe unaitwa nani?” aliuliza yule mzee huku akimuonyeshea kidole hamza.
“hamza”
“sawa, enhe ilikuwaje ukafika katika eneo hili?”
“sijui mzee wangu”
“haujui?, hebu elezea ilikuwaje ukawa katika sehemu hii, yaani tukio la mwasho kulikumbuka?”
“ahnha ni..ni...nili...nilikuwa natoka nyumbani ili kuelekea kwa rafiki yangu ghafla nikiwa njiani nikahisi kuishiwa nguvu harafu kuna upepo nikahisi ulikukwa unavuma sana. Ulikuwa ni upepo mkali sana hali iliyonifanya kufumba macho ili mchanga usije ukaingia machoni. Nilishindwa kukimbia kutokana na kuishiwa nguvu. Baada ya dakika kadhaa nguvu zilirudi na ule upepo ulikuwa umeisha. Nilipokuja kufungua macho, nilistaajabu kwa sababu sikuwepo pale, nilikuwa katika sehemu nyengine, sehemu yenye mazingira ambayo siyafahamu, ni mazingira haya katika sehemu hii!” alimaliza hamza. Ilikuwa ni hadithi ya kustaajabisha kidogo.
Kitaendelea kitu gani, usikose sehemu inayofuata

JINA LA HADITHI – KAZI YA SHETANI
SEHEMU YA         - PILI
MWANDISHI        - ASLAM KHAN
aslamstorymail@gmail.com
aslamstori.blogspot.com

Iliposhia…

Sikujua ni muda gani ulipita mpaka pale usingizi uliponipitia na kulala kabisa. Ila nilikuja kuamka majira ya kama saa nane ama tisa hivi za usiku, hiyo ni kutokana na makadirio yangu tu. Nilistuka sana pale nilipofungua macho. Nilikuwa katika sehemu ambayo sikuifahamu kabisa

Endelea…

Sehemu ngeni machoni kwangu. Sehemu ambayo mazingira yake sikuwahi kuyaona kabla wala kuyasikia yakisimuliwa. Yalikuwa ni mazingira ya ajabu mno kwangu. Yalionekana mazingira yenye rangi nyeupe. Ardhi yake ilikuwa nyeupe kabisa kana kwamba ilikuwa imezingilwa na theruji, badala yake haikuwa theruji
kwa sababu hakukuwa na hali ya maji maji katika ardhi hii wala kiasi cha baridi chenye kufanya ardhi itandwe na theruji, nilistaajabu sana.
Niliangaza huku na huko bila kufanikiwa kuiona nyumba wala watu. Nilikuwa nipo katika sehemu ya jangwa jeupe. Jangwa lisilo na mchanga wala jua kali. Taratibu nilijiinua tokea pale chini na kuanza kutembea kwenda sehemu ambayo sikuwa ninaifahamu. Sikufahamu wapi nilipokuwa ninaelekea kama ndo ulikuwa upande sahihi wala sikufahamu ule ulikuwa ni upande gani wa dira. Sikuliona jua wala mwezi hivyo kushindwa kukadiria kuwa huo ulikuwa ni wakati gani. Kulionekana kuwepo kwa mwanga uliotosha kuyaona mazingira ama watu vizuri lakini hata nilipoangalia juu, sikuweza kuona chanzo cha mwanga huo. Hakuna mbingu ya bluu kama nilivyozoea. Nilitembea taratibu huku nikiendelea kuangalia huku na huko kuona kama naweza kuona hata mtu ambaye angeweza kuyajibu maswali yaliyokuwa yametawala ubongo wangu na ikiwezekana aweze kunipatia msaada, sikuweza kuona mtu.
 Niliendelea kutembea pasi na kujua nini hatma yangu, huku nikiangaza huku na huko bila ya kuona chochote. Baada  ya kutembea  kwa takribani dakika  kama arobaini hivi bila kujua kule nielekeako, ndipo sasa nuru ilipoanza kunijia usoni kwangu. Sio nuru ya mwanga, la hasha! Ni nuru kwa sababu nilianza kukutana na watu wakiranda randa huku na huko. Walikuwa watu wa ajabu sana. Sikuweza kuziona nyuso zao kwa sababu nilikuwa zimetawaliwa na nuru ya ajabu , hazikuweza kutambulika kiurahisi. Nilijikuta nipo katika kiza chenye mwanga. Mwili na mavazi yao yote yalikuwa meupe kabisa kama ambavyo yalivyokuwa mazingira yao. Nilistaajabu na taratibu woga ukaanza kunijia. Nilipiga moyo konde na kujaribu kuwasemesha, lakini hakuna hata mmoja aliyepata kusimama japo kunisikiliza tu achilia mbali kunijibu kwa kunisemesha. Nilizidi kuogopa sana. Nilijikaza kiume na kuendelea na safari yangu huku nikifuata kule ambako kulionekana kuwepo kwa wale viumbe kwa wingi. Nawaita viumbe kwa sababu sifahamu kama ni watu au la! Nilianza kuziona sehemu za makazi ya viumbe hao, lakini ajabu ni kuwa hadi nyumba nazo zilikuwa zikionekana kuwa na rangi ile ile, nyeupe. Hali ile ilinichanganya sana. Ilikuwa hali ngeni nay a kustaajabisha mno. Niliendelea kutembea kwa takribani kilomita moja hivibila ya kupata msaada wa aina yeyote ile. Nikiwa katika hali ya kukata tamaa huku nikiangaza huku na kule, ghafla nilipata tumaini, tumaini jipya, taratibu hofu yangu ilianza kupungua, furaha ikaanza kunijia. Hiyo ni kwa kile nilichokuwa nimekiona, sikuamini macho yangu, nilifikiri labda nilikuwa ninaota, lakini ilikuwa ni kweli, wala haikuwa ndoto.
                                 
                                      ***********************************
Kulionekana kuwepo kwa kikao   au mkutano wa siri miongoni mwa wananchi wa Kopsheng. Wengi wa wananchi hao walionekana walikuwa ni wapingaji wakubwa wa utawala uliokuwa ukitawala katika eneo hilo. Yule aliyeonekana kuwa ni kiongozi wa waasi hao kama ambavyo hujulikana alisimama na kufungua mkutano wakiwa katika sehemu yao ya maficho.
“wapendwa, kwa mara nyengine tena tumekutana hapa kama ilivyo desturi yetu ili kujadiliana juu ya lile suala letu la siku zote lenye kutufanya tukutane hapa….” Alisema akakohoa kidogo na kuendelea
“….wote nafikiri munatambua ni kitu gani kilichotuleta hapa, kwa hiyo siwezi kurudia tena kuelezea ili tujadiliane mambo muhimu, si mutajua muda ni mdogo sana?” Yule kiongozi alisema akiachia swali kwa washirika wa ule mkutano wa siri. Wengi wao walionekana kuitikia kwa kuchezesha kichwa kuonyesha kukubaliana na maneno ya kiongozi wao.
“…..Leo kuna kitu kipya……” alisema  na kuendelea
“….kuna tatizo, tatizo kubwa  sana, kwa uwezo mdogo wa kufikiri inawezekana likaonekana ni tatizo dogo, lakini matokeo mabaya yanaweza kuja kutokea hapo baadae, kwa hiyo nimewaita hapa ili tujadiliane kujua ni kwa namna gani tutaweza kulitatua ingawa nahisi itachukua muda sana!” Alimaliza huku akiwaangalia  washirika wa ule mkutano akiashiria kutaka kusikia neno kutoka kwao.
“Ni tatizo gani tena kiongozi?” aliuliza mmoja wa washiriki wa ule mkutano.
“Je kuna hata mmoja kati yenu ambaye anajua ni kitu gani hasa nilikuwa nimekipanga kukifanya ili kuwasaidia wananchi wetu?” aliuliza.
Ilionekana washirika wa ule mkutano walikuwa wameulizwa swali gumu mno kiasi ya kwamba badala ya kutoa majibu yake, bali ikaanza kusikika ninong’ono  kati yao.
“mmmhgh mmmhg…!” kiongozi alijikohoza baada ya kupita takribani sekunde arobaini na tano za minong’ono. Wote wakanyamaza kimya ili kumsikiliza kiongozi wao.
“…mimi nimeuliza ili nijibiwe, sasa mkianza kunong’ona bila kutoa majibu, tutajikuta muda umetuishia na hakuna cha maana ambacho tutakachokuwa tumekijadili, na badala yake kuonekana mkutano wetu huu hauna faida!” alisema akiendelea kuwaangalia akisubiria jibu.
“hapana..hapana…hapana!” walijibu huku wakisisitiza kuwa hakuna kitu ambacho walikuwa wakikifahamu.
“Tush…!” Yule kiongozi aliita jina la mmoja wa washiriki waliokuwemo ndani  ya eneo la mkutano na alionekana akiinuka na kusimama.
“ndio kiongozi!”
“kwanza  ongera sana kwa kutunza siri hii niliyokwambia juzi na hakuna hata mmoja aneyejua kile nilichokuwa nimekipanga. Naweza kusema kuwa huu ulikuwa ni mtihani mkubwa kwako na naweza kusema kuwa umeufaulu kwa asilimia zote, ongera sana!” 
“ahsante sana kiongozi!”
“ila pia nimestaajabu sana kuona kuwa hata wewe ni umekuwa ni miongoni mwa watu wasiojua kile nilichokipanga!”
“samahani sana mzee!” Tush aliomba msamaha
“huo ndio uamini  wenyewe tunaouhitaji ili kuweza kuichukua nchi hii na kuiweka katika sehemu sahihi zaidi ya hapa tulipo kwa sasa hivi. Uaminifu unauweka mbali usaliti, ooh kwa hiyo hakuna kosa ulilolifanya lenye kukuwajibikia kuomba msamaha Tush, ila nakusifu kwa kile ulichokifanya. Ongera sana!”  alisema na kukohoa kidogo na kuendelea
“Wananchi  wa Kopsheng, mlioamua kuwasimamia wanachi wengi wa nchi yetu hii ambao hawajui nini hatma yao itakavyokuwa kesho, napenda kuwashukuru sana kwa ushirikiano wenu wa karibu  na kufika kwenu kila pale munapokuwa munahitajika. Tunahitajika tushikamane pamoja ili kufanikisha lile tuliloamua kulianzisha kuhusu kinachoendelea nchini kwetu. Sasa kwa kifupi ni kuwa nilikuwa nimepanga kuwaleta viumbe ambao wana uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kutendamambo kwa kutumia akili zaidi kuliko kutenda bila ya kujua matokeo ya matendo yao.” Alisema kiongozi wa waasi.
“Kwa akili zaidi kuliko sisi?” aliuliza mmoja wa washiriki wa mkutano ule wa siri.
“sio kwamba siku zote dawa ya moto ni moto tu, hapana dawa ya moto kwa tafsiri rahisi ni maji, moto ukiwaka chukua maji na uuzime, viumbe hao ni tofauti na sisi, hivyo itakuwa ni rahisi sana kwetu kupata msaada kutoka kwao. Viumbe hao wanao uwezo wa kutafuta mbinu sahihi ya kukitawala kiumbe chochote na kwao hakuna kiumbe kinachowasumbua hasa kama watawezeshwa kwa ufundi Fulani Fulani hivi.” Alisema
“kiongozi wetu, sisi huwa hatukupingi mara nyingi kwani maamuzi ambayo huwa unayachukua huwa na matokeo mazuri baadae, ila swali langu ni kiumbe gani huyo ambaye umefikiria kumleta ili kutusaidia katika suala letu la kuirudisha nchi kule ilikotoka kwenye asili yetu watu wa Kopsheng?” mshirika mwengine aliuliza.
”Binadam, binadam ndio viumbe ambao nimefikiria kuwaleta ili kutusaidia kukabiliana na matatizo yanayotukabili” kiongozi alibainisha.
“binadam?!.....” aliuliza mmoja wao kwa mshangao akaendelea.
Je kwa nini ameuliza kwa mshangao kama hivyo na hao watakuwa ni sahihi au sio?
Fuatilia sehemu inatofuata

 

Jina la Hadithi - Kazi ya Shetani

Sehemu ya       - Kwanza

Mwandishi        - Aslam Khan 

Mawasiliano     - +255 (0) 627 676 104

aslamstorymail@gmail.com

aslamstori.blogspot.com 


Ilikuwa siku ya jumapili moja iliyo tulivu hasa ukizingatia kuwa ilikuwa siku ya mwisho wa juma. Watu walionekana sehemu mbali mbali wakiwa wawili wawili kana kwamba walikuwa wamezaliwa mapacha. Walifurika sehemu mbalimbali za starehe. Watoto nao hawakubakia nyuma nao walionekana wakiranda huku na huko wakiwa na furaha huku wengi wao wakiwa na mapulizo.  Lakini hali ilikuwa ni  tofauti kwa upande wangu kwani siku hiyo nilikuwa nasumbuliwa na homa. Nikiwa peke yangu nyumbani, niliendelea kuwaangalia wapita njia walioonekana kuwa na furaha mno. Hapa nilipokuwa ninaishi, nilikuwa ninaishi mimi pamoja familia ya mjomba akiwepo mkewe na mtoto wao mdogo mwenye umri wa miaka mitano.  Ilipofika majira ya saa kumi alasiri hali ya hewa ilianza kubadilika kwangu, nilianza kuhisi baridi hali iliyonifanya nianze kutetemeka. Nilijitahidi kujikaza ili niyafaidishe macho yangu kutokana na mazingira mazuri ya siku hiyo yaliyopambwa na watu mbalimbali kutokana na rangi zao za nguo. Nilijitahidi kuvumilia lakini nilishindwa hivyo ikanibidi kuingia ndani na moja kwa moja nikaingia chumbani kwangu ili kujipumzisha.  Nilifika chumbani kwangu na kujitupia tu kitandani. Taratibu usingizi wa uchovu na homa ulianza kuninyemelea. Ilipofika takribani saa kumi na mbili kasoro robo, kwa mbali niliwasikia mjomba akiwa na shangazi wakiwa wamerejea kutoka kazini. Baada ya hapo nilipitiwa na usingizi kabisa.

“abdamm.........abdam!” ilikuwa ni sauti ya shangazi akiwa anagonga mlango wa chumba changu.

Wakati huo ilikuwa yapata majira ya saa moja ya usiku. 

“abdam....abdam.....abdam!” shangazi aliendelea kugonga mlango huku akiwa ananiita. Kutokana na uchovu uliotokana na homa niliyokuwa nayo, nilishindwa kumjibu shangazi.

“abdam...abdam!” shangazi aliendelea kuita mara baada ya kuona sijibu kitu.

“naaaa....aaaam!” niliitikia kwa uchovu uliopitiliza.

“njoo ule chakula ili umeze dawa!” shangazi alisema kwa msisitizo.

“mmmmh, haiwezekani chakula kiwe tayari saa moja hii!” niliwaza ila niliamua kumjibu

“naa...anaku...ja” nilijibu kiuvivu.

Zilipita takribani dakika ishirini hivi bila ya mimi kutoka chumbani kwangu wala kitandani. Nilikuwa ninajihisi ni mtu mwenye uchovu mno.

“ngoo...ngo...ngoo”   ilikuwa ni baada ya kupita dakika takribani ishirini sauti ya mlango kugongwa tena ilisikika.

“mmmmmh...mmmmmhhhgg......mmmhhh” nilijigeuza geuza tu pale kitandani niliposikia mlango ukiwa unagongwa.

“abdam!” shangazi alikuja kuita tena.

“mmmmmh....” nilliitikia kwa uchovu.

“amka uje ule chakula!” alisema.

“naa kuja!”

“uje sasa hivi ule chakula cha moto kabla hakijapoa”

“sawa nakuja!” nilijibu huku nikijaribu kuinuka lakini mwili ulikuwa umechoka mno hivyo nikaamua kujipumzisha kidogo ndipo niende nje. Nikapitiwa na usingizi.

                 ******************************************************

“chakula kimechelewa sana leo, mpaka mtoto anataka kulala chakula bado” alisema mjomba mara baada ya kumuona mtoto wake wa kike aitwae Hajra akiwa anasinzia.

“kimechelewa wakati  chakula kipo tayari hapa!” shangazi alijibu

“kimeivaje Wakati bado kipo jikoni hata kupakuliwa bado?” 

“hiki tayari bado kidogo tu”

“ mbona haueleweki, mara tayari mara bado nilielewe lipi sasa, angalia mtoto anataka kulala huyu na sijui kama hata kuoga  kama ameoga!” 

“kwani wote si tumerejea pamoja hapa nyumbani?, wewe muogeshe tu binti yako!”

“oooooh hizo sasa ni dharau nitaanzaje mimi kumuogesha mtoto?”

“kwa nini?”

“mimi ni mwanaume bwana, kumuogesha mtoto na mimi ni wapi na wapi?” aliuliza mjomba kwa mshangao.

“nani aliyesema kama mwanaume hawezi kumuogesha mtoto?” 

“mimi ni mwanaume na siwezi kufanya kazi za kike, umenielewa?”

“kumuogesha binti yako ndo kazi ya kike?”

“Hiyo ni kazi yako”

“hivi wewe mwanaume kumuogesha binti yako ni kazi ya kike, je utaweza kumfulia nguo kweli?”

“hahahahaha hebu usiniletee utani wa kunifurahisha hapa!”

“hivi huwa haumuoni  baba John vile anavyofanya kwa familia yake?”

“anafanyaje?”

“huwa anafua nguo za mkewe, za mwanawe na Wakati mwengine hata kupika pia. Yote ni kumsaidia mkewe, ila mimi hata sina bahati hiyo.”

“hivi nani asiyejua kuwa huyo baba John amewekwa hapa!” alisema mjomba huku akionyesha katikati ya kiganja cha mkono.

“hizo ni imani zenu tu, na ni imani za potofu”

“zipi imani potofu!”

“hizo unazoziamini wewe, hata sijui kwa nini watu huwa munapenda kuwa na imani za kishirikina, yaani mtu kuamua kumsaidia mkewe ili kuijenga familia iliyo bora basi eti karogwa, wangapi sasa watakaokuwa wamerogwa?” 

“hata wakiwa wote!”

“kitabu gani ambacho kiliandika kuwa kufua au kumuogesha mtoto ni kazi za mwanamke?”

“hebu usiniulize hayo maswali yako, fanya haraka umalize kupika nile nikalale!”

“basi naomba tufanye jambo moja!”

“jambo gani?”

“njoo umalizie kupika ili nimuogeshe mtoto!”

“hizo sasa ni dharau zilizopitiliza, ni dharau za reli kiwango cha standard gauge!” 

“mimi sikudharau, ila wewe unaona hivyo, najaribu kurahisisha kazi, njoo upike bwana mume wangu nimuogeshe mtoto basi!” shangazi alisema huku akimuangalia mjomba kimahaba na kufanya macho yake makubwa yaliyo meupe kuongeza urembo wake. 

“aaaah huko sasa ni mbali sana, hebu niandalie tu hayo maji nimuogeshe”alisema mjomba kwa unyonge. Shangazi aliandaa maji kwa ajili ya kumuogeshea mtoto na kisha akampatia mjomba tayari kwa kumuogesha mtoto.

“na hiko chakula ufanye haraka tumpatie mtoto ale, akalale!” alisema mjomba.

“sawa mume wangu!”

“harafu vipi kuhusu abdam?”aliuliza mjomba

“amelala, anajisikia vibaya” 

“aha, sawa kamuamshe kabisa ili aje kusubiria chakula”

“sawa mume wangu ila nilishaenda kumuita kabla, ngoja niende tena!” alisema shangazi na kuinuka kuja karibu na mlango wa chumba changu kwa ajili ya kuniamsha. Aliita bila ya mafanikio, akaamua kwenda kuandaa chakula kwanza.

                         *************************************************

“ngooo.....ngooooo.....ngoooo” ulikuwa ni mlango uliotii kwa kutoa sauti mara baada ya kugongwa. 

“abdam, chakula tayari njoo ule upate kumeza dawa!” shangazi alikuja kuniita tena. Kimya.

“ngooo...ngooo..ngongongo.... abdam....!” shangazi aliendelea kugonga huku akiendelea kuita. 

“mmmmmmmmmh.....” nilijigeuza pale kitandani kutokana na kero zilizotokana na kelele za mlango uliokuwa unagongwa. 

“amka uje ule chakula ili upate kumeza dawa” 

“nakuuu....kuuja” niliitikia katika hali iliyokuwa imetawaliwa na uchovu sana.

“fanya haraka, uje ule chakula cha moto”

“sawa!” nilijibu pasi na kutoka nje. Zilipita dakika kadhaa bila ya kutoka nje.

“ngoongongongo!” ilikuwa ni sauti ya mlango wa chumba changu ukiwa unagogwa lakini safari hii uligongwa kwa nguvu mno.

“abdam hebu toka nje bwana!” ilisikika sauti ya mjomba.

“nakuja mjomba” 

“hebu jikaze, fanya haraka utoke nje uje ule, wewe mwanaume bwana.” Alisema mjomba huku akiendelea kugonga mlango kwa fujo.

“nakuja!” nilijibu huku nikiinuka toka kitandani. Nilitoka nje ya chumba changu na kumkuta mjomba akiwa mlangoni akinisubiria.

“acha kujilegeza, wewe mtoto wa kiume!”alisema mjomba huku akinishika begani na kunitingisha.

“anaumwa bwana, hebu muache huko, kwa nini hauna huruma kwa binadamu wenzako?” shangazi alitetea.

“endelea kumtetea tu, mwanaume huyu, kuna vita, ataweza kupigana huyu?” aliuliza mjomba.

“nina imani ataweza zaidi ya kupambana!” shangazi alijibu na kumfanya mjomba apandwe na hasira. Aliamua kwenda mezani na kuanza kula.

Taratibu na mimi nilielekea sebuleni ili kupata chakula cha usiku.  

“kula umeze dawa”alisema shangazi kwa sauti ya upole iliyojaa huruma.

“acha kumdekeza bwana!” mjomba alidakia.

“haujaacha tu, hebu kuwa na huruma huko”shangazi alitetea.

“endeleeni” alijibu mjomba na kunawa mikono yake.

“kulikoni tena na wewe?”

“nimeshiba”

“umekula wapi, mbona chakula kipo vile vile tu, au tayari umeshakula kwa watu wako huko”

“umeshaanza hivyo!”mjomba alijibu na kuingia chumbani kwake.shangazi hakuwa na neno jengine la kuongezea.

“muache bwana, we kula hapo umeze dawa.” Alisema shangazi huku akizungusha macho yake makubwa na kumfanya aonekane mrembo mno hasa kutokana na mwanga hafifu wa mshumaa.

“sawa shangazi”

Shangazi alikuwa nakula kwa mapozi hali iliyonifanya ubongo wangu upagawe kutokana na mvuto wake aliokuwa nao. Nilikula chakula na nilipomaliza shangazi alinipatia dawa za maumivu na kuzimeza. Nilipomaliza niliingia chumbani kwangu kwa ajili ya kujipumzisha usiku huo.

***********************************************************************************************************                                      

Sikujua ni muda gani ulipita mpaka pale usingizi uliponipitia na kulala kabisa. Ila nilikuja kuamka majira ya kama saa nane ama tisa hivi za usiku, hiyo ni kutokana na makadirio yangu tu. Nilistuka sana pale nilipofungua macho. Nilikuwa katika sehemu ambayo sikuifahamu kabisa. 


Je ni sehemu gani hiyo, usikose sehemu inayofuata. 

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget