Halloween Costume ideas 2015

SHANGAZI I -7


 


Sehemu ya    : SABA (7)

Mwandishi     : Aslam Khan

Mawasiliano  : 0627 676 104

                        0787 378 393

                        0768 965 020

 

Ilipoishia...

 

"Mmh shangazi itakuwa amelala labda!" Nilijisemea kimoyo moyo.

Nilirudi chumbani kwangu na kuvua nguo zangu, na kuchukua taulo kwa ajili ya kwenda kuoga wakati huo haja ndogo ilikuwa imenibana sana nusu ya kutoka yenyewe. Nilikimbilia bafuni ili kuwahi kabla sijadhalilika kwa kujikojolea mtu mzima. Nilifungua mlango wa bafu na kwa haraka nikaingia ndani huku nikiwa tayari nimeshaanza kuushika uume nje ambao ulikuwa tayari umeshaanza kutoa haja ndogo kabla sijafika katika eneo maalum. Nilipoingia bafuni, ndipo haja ndogo ilipoacha kutoka kutokana na mstuko nilioupata. Nilimkuta shangazi akiwa uchi kabisa akiwa anajiandaa kuoga. Niliduwaa, wote tulikuwa kama watu tuliopigwa na shoti, tulibaki tukitazamana kwa muda tukiwa uchi kabisa.

 

Songa nayo...

 

Baada ya kutazamana kwa sekunde kadhaa huku kila mmoja akiwa hajui cha kufanya, shangazi alichukua khanga na kuifunga kiunoni kisha akachukua nguo zake nyengine na kuondoka kuelekea nje pasi na kuongea kitu chochote kile. Nilibakia kule bafuni nikiwa nina waza kile kilichotokea nikiwa natamani nifumbue macho ili iwe ndoto. Baada ya kuwaza kwa muda, niliona hakuna kitu kitakachobadilika, hivyo bora nioge tu. Nilioga huku nikiwa nimejawa na mawazo lukuki. Nilipomaliza kuoga, nilienda chumbani kwangu moja kwa moja na kuvaa nguo zangu kisha kwenda sebuleni. Nilipofika sebuleni, nilimkuta shangazi akiwa amekaa, kitendo cha kufika pale sebuleni, kilimstua shangazi ambaye alionekana kuwa katika dimbwi zito la mawazo. Aliniangalia ila hakunisemesha chochote, kisha akageukia kando kwa aibu. Nikiwa nimejawa na woga, nilikaa katika moja ya viti vilivyokuwepo pale sebuleni nikiwa nina nia ya kuomba msamaha kwa shangazi.

"Shangazi, samahani" nilisema kwa woga ulioambatana na aibu. Shangazi aliinamisha macho yake chini kwa aibu huku akitabasamu na kicheko kilichokuwa kama kinakuja, kinakataa kwa mbali.

"Shangazi nimekosa, tafadhali nisamehe!" Niliendelea kuomba msamaha hali iliyomfanya shangazi kuinua kichwa na kuniangalia. Macho yetu yaligongana na kumfanya shangazi aangue kicheko kilichotawaliwa na aibu. Aliinuka kutoka katika kiti na kwenda moja kwa moja chumbani kwake bila ya kujibu wala kuongea kitu chochote. Nilikaa sebuleni kwa muda nikitafakari kuhusu alichofanya shangazi, kisha niliamua kwenda chumbani kwangu kupumzika, ili kama mawazo bora nikaendelee nayo huko. Baadae nilistushwa na kelele za mlango uliotii amri pale ulipokuwa unagongwa. Nilipoangalia saa ilikuwa ni saa nne kasoro robo. Nilienda kufungua mlango na nikakautana na shangazi ana kwa ana.

"Chakula tayari!" Alisema shangazi huku akiwa ameinamisha macho chini.

"Sawa, nakuja!" Nilimjibu na kuufunga mlango kwa niaba ya kwenda kuongeza nguo nyengine kwani pale nilikuwa na bukta tu pekee. Shangazi alinizuia nisifunge mlango.

"Vipi shangazi?" Nilimuuliza

"Mmmhhmmhh...!" Alikataa kwa kuguna huku akitingisha kichwa na kuondoka. Nilivaa suruali yangu na fulana kisha nikaelekea sebuleni kwa ajili ya kupata chakula cha usiku. Nilikuta shangazi akiwa yeye tayari ameshaanza kula.

"Vipi, mjomba hajarudi?" Nilimuuliza. Shangazi aliniangalia kwa muda kisha akatabasamu na kujifanya kama hajasikia swali langu.

"Shangazi, kwani mjomba hajarudi?"

"Ndio hajarudi!"

"Mpaka muda huu, saa nne hii" niliuliza kwa mshangao

"Ndio, kula kwanza Abdam!" Alisema shangazi huku akiwa anakula kwa mapozi. Nilianza kula kile chakula huku nikijiuliza maswali mengi hasa kwa nini shangazi nimemuomba msamaha lakini hajanijibu na badala yake aliondoka tu. Au labda atakuwa amekasirika sana. Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.

"Shangazi, samahani,kwa kile kilichotokea leo!" Baada ya kimya cha muda mrefu, nilianzisha tena mazungumzo.

"Usijali!" Shangazi alijibu kwa mkato.

"Niambie kama umenisamehe!"

"Nitakujibu usiku, sasa hivi kula kwanza!"

"Usiku si ndo huu shangazi lakini!"

"Subiri, tutaongea!"

Tukiwa tunaendelea kula, ghafla simu ya shangazi ilitoa mlio kushiria kuwa kulikuwa na ujumbe mfupi wa maneno ulikuwa umeingia. Aliinua na kuiangalia kwa muda

"Wooow..!" Alisikika shangazi akisema bila ya kutegemea kiasi mpaka nikastuka na kumuangalia.

"Vipi tena?" Nilidadisi

"Shika usome mwenyewe!" Alisema shangazi na kunipatia simu yake ili nisome ule ujumbe uliokuwa umeingia

"SAMAHANI DEAR KWA KUCHELEWA KURUDI MPAKA SASA HIVI. ILA NIMEPATA KAZI MPAKANI AMBAYO INAWEZA IKANIWEKA HUKU KWA SIKU TATU MPAKA TANO. MWANZO NILIJUA NI KAZI NDOGO, ILA NILIVYOFIKA HUKU, NIMEKUTA NI KUBWA. MTUNZE MJOMBA ASIJIONE MPWEKE. NAKUPENDA SANA MKE WANGU NA HAKIKISHA KITUMBUA CHANGU HAWACHEZEI WATOTO KIKAINGIA MCHANGA, USIKU MWEMA" Nilimaliza kusoma na kumrudishia simu yake.

"Sasa siku tano mbona nyingi sana hivyo?" Niliuliza

"Mbona mimi nimeshazoea, kuna wakati inafikia hadi wiki mbili mpaka miezi sita"

"Mwezi?"

"Ndio, ndo hivyo!"

"Duh!"

Wakati huo nilikuwa tayari nimeshamaliza kula. Nilimuuliza shangazi wapi vinapowekwa vyombo vichafu.

"Hamna, wewe viache tu hapa, nitavitoa!"

"Sawa, basi mimi naenda kupumzika shangazi!"

"Heee na wewe, upo kama mjomba 'ako?"

"Kwa nini?"

"Mjomba wako na yeye ndo hivyo hivyo, akimaliza kula tu, ananiacha peke yangu!"

"Kumbe ndo tabia yake eeeeh!" Nilitania

" tabia yake au tabia yenu, ukoo wenu!"

"Basi mimi nitakusubiria mpaka nitapohakikisha unazima hadi taa zote za sebuleni!"

"Unaweza?"

"Ndio naweza, subiri uone!"

 

Unafikiri ni kitu gani kitakachotokea?


Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget