Halloween Costume ideas 2015

SHANGAZI II -9


 Jina la hadithi.   : SHANGAZI II

Sehemu  ya       : TISA (9)

Mwandishi        : Aslam Khan

mawasiliano     : aslammusamail@gmail.com


Ilipoishia...


"Mmmh hili giza linaninyima raha!" Niliwaza moyoni mwangu.

"Labda nijaribu kuingiza vidole ndio nitapata uhakika!" Niliendelea kuwaza. Niliviandaa vidole vyangu viwili kwa kuvipaka mate yaliyochanganyika na ute ute uliotoka ukeni ili niviingize katika uke wa Husna, hivyo ndo ningepata uhakika. Niliendelea kulamba kisimi chake huku nikijiandaa kwa kile nilichokidhamilia...


Endelea...


Niliviandaa vidole vyangu na kuanza kuhesabu kimoyomoyo.

"Moja....mbili....tat....!" Niliviingiza vidole, lakini havikuingia. Husna aliruka juu na kuinuka kutoka kwenye kiti.

"Abdam, kwa nini lakini?" Aliniuliza huku akiniangalia kwa jicho lililoregea kutokana na msisimko wa mwili wake.

"Samahani Husna, nisamehe sana!"

"Nijibu, kwa nini umeamua kuniumiza, unakumbuka nilikwambia nini tangu mwanzo?"

"Nikumbushe!"

"Nilikwambia mimi sijawahi kufanya mapenzi na mwanaume tangu nizaliwe, sasa unapotaka kunifanyia hivyo hujui kama utaniumiza, tena vidole viwili, angalau kingekuwa kidole kimoja. Kwani bikra ndo huwa inatolewa hivyo au hauniamini kile nilichokwambia?"

"Samahani Husna, nisamehe bwana!" Nilijibu huku nikimsogelea na kumshika kiuno kwa kumkumbatia.

"Hebu niache, niache Abdam tafadhali. Leo nilitaka nikupe penzi na uitoe bikra yangu, lakini umefeli mtihani mdogo tu kutokana na papala zako, kwa leo inatosha mpaka siku nyengine!"

"Husna, usifanye hivyo bwana!"

"Muda umeenda sana sasa hivi, chukua nguo zako uvae na uende ukalale!" Husna alisema huku akiwa anaanza kuvaa nguo zake. Niliona kweli Husna alishakusudia kuwa shughuli ilikuwa imeishia pale. Nilijilaumu kwa haraka yangu ya kutaka kuthibitisha, na kujifanya mchunguzi.

"Husna..." 

"Vaa uondoke, ulichokifanya ni kukosa kujiamini na kukosa kuniamini mimi pia, vaa!" Alisema Husna wakati huo yeye alikuwa ameshamaliza kuvaa. Nilichukua nguo zangu na kuzivaa. Nilipomaliza, nilianza kuondoka kwenda nje.

"Kuna zawadi yako nilikuandalia!" Husna alisema. Niligeuka ili kuiona hiyo zawadi. Husna alifungua friji na kutoa keki iliyokuwa ndani ya boksi lake.

"Zawadi yangu, kwani ulijua kama nitakuja, itakuwa ulijinunulia mwenyewe tu harafu unataka kunidanganya!"

"Ndio, nilijinunulia mwenyewe, nimeamua kukupatia, je umeridhika?" Alisema huku akinipatia boksi lenye keki.

"Hata nisiporidhika, nitafanya nini sasa!"

"Naona haupo sawa, ngoja nikupatie na juisi labda ukifika kwenu utataka kula hiyo keki, kwa hiyo utashushia na juisi!" Husna alisema huku akichukua chupa iliyokuwa na maji na kuyamimina kisha akachukua juisi kwenye jagi na kuimiminia kwenye ile chupa.

"Hii hapa, nahisi itakutosha!" Alisema Husna na kunipatia ile chupa ya lita moja.

"Itatosha tu, ahsante sana!"

"Usijali, ngoja nikusindikize!"

"Tulitoka ndani na kuanza kutembea taratibu kuelekea nyumbani. Nilisikia kelele za malumbano chumbani kwa Thomas lakini sikutaka kusikiliza kilichokuwa kinawafanya wagombane mtu na mpenziwe.

"Abdam!"

"Naam!"

"Unajua kwenye maisha, unatakiwa kuwa mvumilivu, mstaarabu na mwenye subira. Ukiwa na vitu vyote hivyo, itakuwa ni rahisi kupata vitu vizuri au hata unavyovihitaji!"

"Nimekuelewa..!"

"Umenielewa au ndo unataka nimalize kuongea?"

"Usijali, nimekuelewa Husna, harafu hapa uliponisindikiza panatosha, rudi ukapumzike!"

"Ngoja nikusindikize mpaka paleee harafu narudi, sawa my?"

"Hamna, wewe rudi bwana, harafu nimekumbuka, Husna, unafanya kazi gani?"

"Hahahah kuwa na subira, utajua kama utakuwa mvumilivu, kama utakuwa na subira pia kama utakuwa mstaarabu na mpole!"

"Mbona unapenda kunizungusha zungusha wewe, unajua sikuelewi!"

"Inaonekana una haraka sana Abdam, kumbuka haraka haraka haina baraka!"

"Lazima nijue, nisije kuwa na mtu kumbe kazi yake kubwa ni kudanga, harafu nikaja kupata magonjwa bure!"

"Abdam, nitake radhi!"

"Radhi ya nini, kama haufanyi hivyo mbona unaogopa kuniambia kazi yako!?"

"Nakwambia niombe msamaha!"

"Msamaha wa nini sasa?"

"Haujui unachokiongea, haukijui?"

"Nawe kwa nini hautaki nijue kazi unayoifanya!"

"Muda haujafika, muda wa kujua kazi ninayoifanya haujafika!"

"Sasa hiyo kazi gani ambayo haitajwi mpaka ufike muda maalum?"

"Unataka kuifahamu kazi ninayoifanya?"

"Ndio!"

"Ukinioa ndo utaifahamu. Kesho nitakwambia ndugu zangu walipo upeleke posa!"

"Khaaa posa tena, hata kazi sina, hela sina harafu nipeleke posa si maajabu tena hayo?"

"Mimi naelewa yote hayo na ndio maana nikakuambia kuwa mvumilivu, mpole na mstaarabu. Lakini naona kama unataka kushindwa!"

"Basi sawa, yaishe, wewe rudi tutaongea kesho!"

"Sawa Abdam, usiku mwema, mwaaaaah!" Alisema Husna huku akinibusu mdomoni.

"Nawe pia!"

"Sikiliza Abdam, kama kutakuwa na tatizo lolote lile, usisite kunijulisha harafu tutaangalia tunasaidiana vipi!"

"Sawa Husna!"

"Jamani, hata kuniita mpenzi hutaki!"

"Usijali, nenda kapumzike!". Niliachana na Husna, nami nikaingia ndani.

"Nani huyoo?" Sauti ya baba ilisikika.

"Mimi"

"Mimi ndo nani?"

"Abdam!"

"Usiku huu unatoka wapi, na nilikutafuta sana kuna tatizo hapa nyumbani!"

"Kuna mzigo nilienda kuuchukua kwa rafiki yangu!"

"Basi kama ni hivyo, sawa. Maana mjomba wako amesema usafiri kesho manake yeye anataka kwenda sehemu kikazi. Kwa hiyo, hiyo wiki ijayo anaweza akawa kazini. Hivyo inabidi kesho usafiri kwa gari za saa tano!"

"Heee mbona ghafla hivyo!"

"Amenipigia simu usiku huu huu!"

"Hata nguo sijafua!"

"Utaenda kufulia huko huko!"

"Sawa baba!"

Niliingia chumbani kwangu na kwa haraka niliifungua ile keki.

"NAKUPENDA SANA ABDAM!" Yalikuwa ni maneno niliyoyakuta juu ya keki. Pembeni kulikuwa na karatasi iliyoandikwa ujumbe. Niliifunua na kusoma

"ABDAM, KESHO NAENDA KAZINI KUFUATILIA BAADHI YA MIPANGO YANGU. BIKRA YANGU NI MALI YAKO, HIVYO NATARAJIA KUKUPATIA KESHO KUTWA. NAKUPENDA SANA!"

Nilipomaliza kusoma moyo ulinipiga na kujikuta miguu ikifa ganzi. Macho yalinitoka mithili ya mjusi aliyebanwa na mlango.


Kipi kitatokea..

Itaendelea...

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget